Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, akiwa katika mazungumzo na Ujumbe wa Umoja wa Ushirikiano na Nchi za Nje wa Wataalam wa masuala ya Kilimo na Mifugo kutoka Fujian China, leo, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni kiongozi wa Ujumbe huo Li Lin.
Baadhi ya wajume wakitazama kipeperushi hicho
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akimkabidhi zawadi maalum Mkuu wa Msafara wa ujumbe wa Umoja wa Ushirikiano na Nchi za Nje wa Wataalam wa masuala ya kilimo na Mifugo kutoka Fujian China, Mwenyekiti wa Umoja huo, Li Lin, baada ya mazungumzo hayo
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akikabidhiwa zawadi maalum na Mkuu wa Msafara wa ujumbe wa Umoja wa Ushirikiano na Nchi za Nje wa Wataalam wa masuala ya kilimo na Mifugo kutoka Fujian China, Mwenyekiti wa Umoja huo, Li Lin, alipowasili ukumbini tayari kwa mazungumzo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...