Ikiwa ni takribani mwaka na usheee sasa tangu kuanza kwa utaratibu mpya wa matumizi ya Barabara za Jijini Dar es salaam, lakini bado kumekuwa na changamoto katika eneo hili la Faya kwani kuna madereva bado wanatumia utaratibu ule ule wa awali. Kamera yetu leo iliangazia eneo hilo la Faya na kukutana na hali hii ya upishanaji wa magari ambao si salama kabisa kwa watumiaji wa barabara hiyo. Jambo hili limekuwa limekuwa likiendelea kufanyika kimazoea maana si gari moja au mbili zinazotumia utaratibu ule wa awali (Ukiangalia picha hizi utabaini kinachoelezwa hapa) Maana unakuta taa zimeruhusu kwa gari zinazokenda moja kwa moja, halafu ghafla tu unakutana na gari lingine likikatisha mbele yako kuelekea upande mwingine. hiki ni kijipu upele ambacho kikija kutumbuka balaa lake litakuwa si dogo, hivyo inapaswa litafutiwe ufumbuzi sasa, na kuna umuhimu wa kutoa mafunzo ya kutosha kwa matumizi ya barabara hizi.
 Hivi ndivyo mambo yanavyokuwa pale taa za kuongozea magari zinaporuhusu magari yananyokwenda moja kwa moja lakini wengine hukatisha ghafla namna hii.
Inafika wakati gari zinazokwenda moja kwa moja zinalazimika kusimama katikati ya barabara ili kupisha zinazokatisha ambazo ziko nje ya utaratibu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Asante mdau kwakuliona hili pale panachanganya sana zile taa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...