Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Gift Msuya.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi jijini Dar es Salaam leo.

Na Yassiri Adam, Globu ya Jamii.
WILAYA ya Kinondoni imezindua kampeni ya wajasiriamali kwa vijana ili kuweza kutatua changamoto ajira kwa vijana na wananchi wa Wilaya hiyo.

Akizungumza na watendaji wa Wilaya hiyo wakati wa uzinduzi kampeni ya ujasiriamali, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amesema kuwa wananchi wakipata mafunzo ya ujasirimali itasaidia fursa kuongeza ajira kwa vijana.

Amesema mapato mengi yanayokusanywa kwa wilaya ya Kinondoni yanatokana na watu walioweza kujiajiri wenyewe wakaweza kuajiri watu wengine.

Hapi amesema kuwa vijana wakipata mafunzo ya ujasirimali kutasaidia kuondokana na kujiingiza katika vitu visivyo ikiwemo maandamano yasiyokuwa na tija , kujiingiza katika makundi ya uhalifu pamoja uzurulaji.

Aidha amesema kuwa mafunzo hayo yataanza kwa walimu 30 ambao wakimaliza mafunzo hao watafundisha vijana wengine katika maeneo mbalimbali ujasiriamali wa kilimo cha mbogamboga, mama lishe ,ufugaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...