Warembo wa Miss Ilala 2016 wakiwa katika picha ya pamoja.
**************

SHINDANO la Kumsaka Miss Ilala 2016 linafanyika leo katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency – Kilimanjaro, jijini Dar es Salaam.

Mbali na kufanyika kwa shindano hilo pia litatumika kuadhimisha miaka 20 ya shindano la Miss Ilala tangu kuanza kufanyika kwake na warembo mbalimbali waliowahi kushiriki na kushinda taji hilo watahudhuria.

Mratibu wa shindano hilo, Erick Othman kutoka Kampuni ya Gogetime Enterprises ya jijini Dar es Salaam, alisema kuwa warembo 14 watapanda jukwaani kuwania taji hilo pamoja na tiketi ya kushiriki shindano la Kitaifa la Miss Tanzania 2016 linalotaraji kufanyika baadae mwaka huu.

Othman alisema mgeni rasmi katika shindano hilo leo hii ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, huku burudani ikitolewa na wasanii mbalimbali akiwepo Rubby.

Amewataja warembo wanaoshindana kuwania taji hilo kuwa ni Osmunda Mbeyela, Mercy Zephania, Melody Tryphone, Dalena David, Nuru Kondo, Julitha Kabete, Sporah Luhende, Queen Nazil, Lilian Omolo, Mariam Maabad, Brenda Allan, Sabrina Halifa, Agriphina Nathaniel na Grace Malikita.

Kwa upande wa zawadi za washindi, Kitundu alisema kuwa mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita cha sh milioni moja pamoja na portable TV kutoka Startimes, huku mshindi wa pili akipata sh 700,000 na kingamuzi, na mshindi wa tatu akipata sh 300,000 na kingamuzi pia.

Alisema kuwa mshindi wan ne atapata sh 200,000 na watano atapata sh 150,000 pamoja na kingamuzi huku warembo wengine watapata kifuta jasho cha sh 50,000.

Kiingilio katika shindano hilo ni Sh 50,000 kawaida na Sh 100,000 kwa viti maalum (VIP).

Wadhamini ni Coca cola, Atsko, Darling, Channel 10, Kitwe General Traders, Uefa Goo, Mustafa Hassanali, Majira, High Spirit, StarTimes, Father Kidevu Blog na wengineo.
Washiriki wa Miss Ilala 2016 wakiwa katika picha baada ya mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. warembo hao wanataraji kupanda jukwaani Septemba 9, 2016 katika Hoteli ya Hyatt Regency – Kilimanjaro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...