Pazia la
michuano Taifa ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising
Stars jana lilifunguliwa katika uwanja wa Kukumbukumbu ya Karume jijini Dar es
Salaam ambapo timu
ya wavulana ya Temeke ilitoa onyo kali kwa timu shiriki kwa kuifunga Kinondoni
4-1.
Mchezo huo ulitanguliwa na mechi ya wasichana kati ya Arusha na
Lindi ambapo Arusha waliibuka na ushindi wa 2-0. Magoli ya Arusha yalifungwa na
Eva Michael dakika ya 39 kwa njia ya penati na pili likifungwa na Warda Alfonce
dakika ya 60.
Katika mchezo wa Temeke na Kinondoni, Temeke walianza kwa kasi ya
aina yake na kupeleka mashambuliazi ya mara kwa mara langoni mwa Kinondoni huku
Kinondoni wakionekana kuzidiwa katika kila idara.
Temeke waliandika bao la
kwanza kupitia kwa Ramadhan Kawambwa kaika dakika ya 14, kwa njia ya penati
baada ya mchezaji wa Temeke kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari. Goli hilo
lilipokelewa kwa shangwa na mashabiki wa Temeke.
Temeke awalipata bao lao la pili kupitia kwa Abirahi Uihuro mnamo
dakika ya 34 ambaye aligongeana mpira kwa uzuri na Ismail Kovu na kisha
kumchambua kipa wa Kinondoni kwa umaridadi wa hali ya juu na kuukwamisha mpira
huo kimiani.
Mohammed Mbegu aliifungia Temeke bao la tatu katika dakika ya 40
na kuzidi kuzamisha jahazi la Kinondoni ambao walinekana kama vile wamesimama
wakati mchezo ukiendelea.
Rosea Mpoma aliwaliza kwa mara nyingine tena Arusha baada ya
kuifungia Temeke bao la tano katika dakika ya 53 baada ya kuachia shuti kali na
kuzama moja kwa moja wavuni.
Alikuwa ni Abirahi Uihuro tena, ambaye aliiandikia Temeka bao la
nne mnamo dakika ya 28 ya kipindi cha pili baada ya kuunganisha krosi
iliyochongwa na Mohammed Mbegu kutoka upande wa kushoto mwa uwanja na
kuendeleza karamu ya magoli kwa Temeke.
Kinondoni walipata goli ya kufuta machozi mnamo dakika 36,
likifungwa na Shaban Mangula baada ya mabeki ya Temeke kushindwa kuokoa mpira
wa kona.
Michuano hiyo ya Airtel Rising Stars itaendelea kesho kwenye
uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam na kufikia tamati Jumapili, Septemba 11.
Mshambuliaji
wa Arusha, Jenifa Veina (kulia) akijaribu kufunga huku kipa wa Lindi akijaribu
kuzuiya katika mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa
Karume jijini Dar es Salaam jana.
Mchezaji
wa Arusha, Diana Mosses (kulia) akiwania mpira na beki wa Lindi , Neema Hashim katika
mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar
es Salaam.
Kiungo
wa timu ya Arusha,Joyce Faraja (kulia) akiwatoka wachezaji wa Lindi katika
mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar
es Salaam
Kiungo
wa timu ya Arusha,Joyce Faraja (jezi namab 13) akiwatoka wachezaji wa Lindi
katika mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars kwenye Uwanja wa Karume
jijini Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...