Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa
akilihutubia Bunge kabla ya kutoa kauli ya kuliahirisha bunge hilo mpaka
tarehe 1 Novemba 2016 ambapo mbali na mambo mengine amesema serikali
itaendelea kutekeleza yale iliyoyaahidi na kuwashukuru wadau mbalimbali
wanaoendelea kujitolea kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani
Kagera, wakati wa kikao cha nane cha Bunge la kumi na moja la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wakiimba wimbo wa taifa baada ya Waziri Mkuu kuliahirisha Bunge hilo mpaka tarehe 1 Novemba 2016, Leo Mjini Dodoma.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Mhandisi Gerson Lwenge akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali itahkikisha inaipa kipaumbele miradi ya maji ambayo haikutekelezwa kwa awamu ya kwanza, wakati wa kikao cha nane cha Bunge la kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mhe. Abdalah Ulega (katikati)akiwaeleza jambo Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, wakati wa kikao cha nane cha Bunge la kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mhe. James Mbatia akimueleza jambo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa kikao cha nane cha Bunge la kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...