Spika wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja ambapo pia alisema kiasi cha shilingi milioni themanini na tano na laki tano zimechangwa kutokana na makato ya posho ya siku moja yawabunge kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
 Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira, Vijana na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (MB) picha juu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali bungeni ambapo alitoa wito kwa wabunge kuisaidia kutoa elimu kwa wananchi waliovamia maeneo ya jeshi kuondoka ili kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Jumanne Maghembe (MB) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula (MB), wakati wa kikao cha saba cha Bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule akiuliza swali bungeni kutaka kujua mikakati ya serikali katika kutatua migogoro baina ya wakulima na wafugaji inayopelekea mauaji ya raia ambapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi alisema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaohusika na mauaji ya raia nchini hasa ikiwemo wanaohusika kwenye migogoro hii.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...