Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), Freeman Aikael Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James
Mbatia leo wamewatembelea Waathiriwa wa
Tetemeko na kuwafariji Bukoba. Pia waliambatana na Mbunge wa Viti
Maalum Bi. Savelina Mwijake, Mbunge wa Bukoba Mjini, Mh. Rwakatare pamoja na Viongozi mbalimbali.
Mhe. James Mbatia Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi ambae
ni Mtaalamu wa Masuala ya Maafa amewaunga
mkono Wanabukoba leo akiambatana na Mwenyekiti mwenza Taifa na Kiongozi
wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mhe.Freeman Mbowe kwenye safari ya
kuwatembelea wahanga. Katika Safari hiyo wametoa misaada ya dharura kwa
wahanga ikiwemo chakula, sukari, fedha na n.k, wataendelea na safari hiyo kuwatembelea Wahanga hapa Mkoani Kagera
katika sehemu mbalimbali. Leo wametembelea sehemu ya Kibeta, Hamugembe,
Kashozi, Nshambya katika shule ya Ihungo iliyoathiriwa zaidi na Tetemeko
hilo kubwa la Ardhi na kuwafanya wanafunzi kusimamisha masomo yao kwa
wiki mbili kwa kukosa sehemu ya kusomea/Madarasa na Mabweni.
Sehemu ya Majengo katika Shule hiyo kwa sasa baada ya kutokea Tetemeko
Tetemeko likiwa limeharibu sana sehemu kubwa ya Kanisa katika Shule hiyo ya Ihungo iliyopo kilometa 8 kutoka Bukoba Mjini
Taswira ya sasa Wanafunzi wa Shule ya Ihungo wakijipanga kuondoka
Majumbani mwao baada ya Tetemeko la jumamosi kuwaathiri kiasi kikubwa na
kushinikizwa kufunga shule hiyo kwa wiki mbili kupisha kuangaliwa upya
kwa Shule hiyo kutokana na kuathiriwa na tetemeko.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...