Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kaluwa akinadi vitu mbalimbali katika harambee hiyo kuchangisha fedha za ujenzi wa kituo cha kutoa huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu eneo la Tegeta, harambee iliyoendeshwa na Kanisa la Deliverance Centre Victorius (CVC), chini ya Mchungaji Jehu Mkono. Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kaluwa akizungumza katika harambee hiyo kuchangisha fedha za ujenzi wa kituo cha kutoa huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu eneo la Tegeta, harambee iliyoendeshwa na Kanisa la Deliverance Centre Victorius (CVC), chini ya Mchungaji Jehu Mkono.

 MBUNGE wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kaluwa ameongoza harambee ya uchangishaji wa fedha za ujenzi wa kituo cha kutoa huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu eneo la Tegeta, harambee iliyoendeshwa na Kanisa la Deliverance Centre Victorius (CVC), chini ya Mchungaji Jehu Mkono. Harambee hiyo ilifanyika katika Kanisa la Deliverance Centre Victorius Tegeta kwa Ndevu, jijini Dar es Salaam, ambapo Bonnah Kaluwa alikuwa mgeni rasmi na kufanikiwa kukusanya fedha shilingi 13,730,000 ambazo zilipatikana kwa michango ya waumini, wageni waalikwa na kufanyika kwa mnada ulionadi vitu anuai.

 Katika harambee hizo Mbunge, Kaluwa alitoa shilingi milioni mbili yeye pamoja na mumewe huku akiendesha mnada uliotunisha mfuko wa ujenzi wa kituo hicho. Awali akizungumza katika harambee hiyo Mwenyekiti wa umoja wa akinamama wa kanisa la CVC, Rose Haji Mwalimu alisema harambee hiyo itawezesha kupatikana kwa fedha za ujenzi wa kituo pamoja na upanuzi wa kanisa la CVC eneo la Tegeta mradi unaotarajia kutumia shilingi milioni 40.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...