Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umewahimiza madereva wa boda boda kujiunga na mfuko huo ili kuwa na uhakika wa kupata matibu wakati wote.
Wito huo umetolewa na Afisa Mawasiliano Mkuu wa NHIF, Bwana Luhende Singu alipokuwa akizingumza na waendesha boda boda wanaoshiriki katika mashindano ya Kombe la Kamanda Mpinga yanayeondelea katika Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa.
Amesema kupitia mpango wa bima ya afya kwa wajasiliamali (KIKOA), waendesha boda boda hao waliojiunga katika vikundi vya wajasiliamali vilivyosajiliwa, wanaweza kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Ameongeza kuwa mpango huo unawapa fursa waedesha boda boda kupata huduma za bima ya afya kwa kuchangia shilingi 76,800/- kwa mwaka kwa kila mwanachama.
Bwana Singu amesisitiza kuwa kutokana na kazi zao ambazo zinawaweka katika mazingira ya ajali mara kwa mara ni muhimu waendesha boda boda hao wakajiunga na bima ya afya ili kuepukana na gharama za matibabu wanazokabiliana nazo hivi sasa mara wanapohitaji matibabu.
Mashindano ya Kombe la Mpinga yanashirikisha timu zinazoundwa na Waendesha boda boda katika Manispaa ya Ilala ambapo zaidi ya timu mia moja zinawania kombe hilo.
01-2Afisa Mawasiliano Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Bwana Luhende Singu akizungumza na waendesha boda boda kuhusu kujiunga na mfuko huo ili kuwa na uhakika wa kupata matibu wakati wote leo katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mawasiliano Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Bwana Luhende Singu akizungumza na waendesha boda boda kuhusu kujiunga na mfuko huo ili kuwa na uhakika wa kupata matibu wakati wote leo katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mawasiliano Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Bwana Luhende Singu akizungumza na waendesha boda boda kuhusu kujiunga na mfuko huo ili kuwa na uhakika wa kupata matibu wakati wote leo katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Maafisa wa NHIF wakiwa katika picha ya pamoja na waendesha boda boda wanaoshiriki katika mashindano ya Kombe la Kamanda Mpinga yanayeondelea katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Picha na Emmanuel Masaka, Globu ya Jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...