Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam,Mkurugenzi Mkuu wa Society Watch, Simon Mnkondya wakati wa kukabidhi cheti utambuzi wa kazi ya msanii Kallah Jeremiah kushirikisha watoto katika wimbo wana ndoto, amesema kuwa watoto yatima wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo kunahitaji jitihada za kuweza kusaidia watoto yatima.

Mkondya amesema kuwa mpango wa utaoji wa elimu kwa serikali kwa kundi hilo inawezekana kutokana na uchache. Amesema kuwa watoto yatima wamepata hamasa kwa wimbo wa Mwanamziki wakikizazi kipya Kala jeremiah ''wanandoto'' ambapo taasisi hiyo imeliona kundi hilo linalo umuhimu wakipekee yakutoachwa nyuma katika suala la kupata elimu .

''Hamasa ya taasisi yetu Society Watch nikuwasaidia watoto yatima walipo vijijini katika kupata elimu hasa kwa watoto wanaishi katikamazingira magumu katikamaeneo yavijijini ,hamasa hii imetokana na wimbo wa wanandoto wakala jeremamiah kwani watoto hawa wanao mchango mkubwa katika kulitumikia taifa ''Alisema Mkurugenzi Simon Mkondya.

Amesema kuwa kutokana na msanii huyo wakizazi kipya Kala jeremiah kuona umuhimu watoto yatima kupewa fusra yakupata elimu kama watoto wengine kupitia wimbo wanandoto unalenga kuihamasisha jamii kulisaidia kundi hilo maalum katika kupata elimu .

Mkondya amesema serikali inaowajibu wakipekee katika kuwasaidia watoto yatima kuwawezesha kundi hilo kuweza kupata elimu kwani kutokana naumuhimu wawatoto hao katika kujenga taifa nakuliletea taifa maendeleo katika hazina yaviongozi wakesho ,hivyo serikali najamii inawajibu wakulisaidia kundi hilo katika kuwapatiaelimu.

Nae Msanii wa kizazi kipya nchini Kallah Jeremiah amesema kuwa yeye pamoja nawanamziki wa kizazikipya wameimba wimbo huo''wanandoto'' kuikumbusha serikali kuwaasaidia watoto yatima walipo katika mazingira magumu kuwa wanao umuhimu wakipekee katika kupata elimu . Amesema kuwa ni mara kwanza kwa watu kumpa cheti kwa kukubali kazi anayoifanya katika jamii.

Mkurugenzi Mkuu wa Society Watch, Simon Mnkondya akimkabidhi Kallah Jeremiah cheti cha utambuzi wa kazi ya msanii Kallah Jeremiah kwa kushirikisha watoto katika wimbo wana ndoto, leojijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Society Watch,Issabela Liso .


Mkurugenzi Mkuu wa Society Watch, Simon Mnkondya akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kukabidhi cheti cha utambuzi wa kazi ya msanii Kallah Jeremiah kushirikisha watoto katika wimbo wana ndoto, leojijini Dar es Salaam.kushoto ni Msanii wa kizazi kipya nchini Kallah Jeremiah .

Msanii wa kizazi kipya nchini Kallah Jeremiah akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuushukuru uongozi wa Society Watch kwa kumpa cheti kwa kukubali kazi anayoifanya katika jamii.kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Society Watch, Simon Mnkondya
KATIKA kuhakikisha watoto yatima hawaachwi nyuma katika suala zima la elimu nchini ,Taasisi ya Society Watch imeanzisha kampeni maalum kundi hilo kutokana na watotot yatima kuwa changamoto mbalimbali zinazofanya ndoto zao zishindwe kutimia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...