Na Eleuteri Mangi na Beatrice Lyimo, MAELEZO, Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye amewataka wadau wa habari na wananchi
kwa ujumla kutoa maoni juu ya Muswada wa Sheria ya Huduma ya Habari wa
mwaka 2016 uliosomwa kwa mara ya kwanza Bungeni leo mjini Dodoma.
Akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kuhairishwa Bunge, Waziri Nape amesema kuwa muswada
huo unalengo la kuboresha tasnia ya habari ili kuweza kurahisha
utendaji kazi wa wanahabari na kuifanya tasnia hiyo kuheshimika nchini.
“Ombi langu kwa wadau wa tasnia
hii wausome vizuri muswada huo na kujitokeza kwa wingi na kutoa maoni
yao ili tuwe na sheria itakayoleta magezuzi na kukuza tasnia ya habari”
amesema Waziri Nape.
Waziri Nape amewataka wadau wa
habari kuendelea kusoma muswada huo ili kuweza kupata mapendekezo ya
namna ya kuifanya sheria hiyo kuwa bora kwa manufaa ya maendeleo ya
taifa.Aidha, Waziri Nape amewaahidi
wadau wa habari kukutana nao mara kwa mara wakati wa kutoa maoni na
mapendekezo yao yatakayosaidia kuboresha mazingira ya wanahabari nchini
ili waweze kufanya kazi yao ipasavyo wakati wa kutekeleza majukumu yao
ya kuhabarisha umma.
Vile vile, Waziri Nape
amewapongeza waandishi wa habari kwa kushiriki vema katika kuhabarish
umma kuhusu mkutano wa Bunge uliohitimishwa leo na kuahidi kuendelea
kushirikiana nao wakati wote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...