YAH: KUKANUSHA
TAARIFA INAYOSAMBAZWA KWENYE
MITANDAO MBALIMBALI
YA KIJAMII
Ofisi ya Makamu wa Rais inakanusha taarifa inayosambazwa kwenye
mitandao ya kijamii kwamba Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama
Samia Suluhu Hassan, ameomba kujiuzulu nafasi yake na kwamba taarifa hiyo ni ya
uzushi na uongo haina ukweli wowote.
Taarifa hiyo ni ya uchochezi inayolenga kuliweka Taifa kwenye
taharuki. Mhe. Makamu wa Rais yuko bega
kwa bega na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanya kazi
zao kwa mujibu wa Katiba ya nchi ili kuwaletea wananchi maendeleo.
Ofisi ya Makamu wa Rais inawataka wananchi na Watanzania kwa ujumla
kupuuza taarifa hiyo ambayo inalenga kupotosha umma kuhusu ushirikiano mzuri
uliopo baina ya Viongozi wetu.
Mwisho, Ofisi ya Makamu wa Rais inawasihi Watanzania kufanya kazi kwa
bidii na wajiepushe na vitendo vinavyolenga kuvuruga amani na utulivu nchini.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...