Mama Tereza hivi sasa
anajulikana kama Mtakatifu Teresa wa Calcuta, baada ya kutawazwa rasmi na
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis.
Leo maelfu ya watu
wamejitokeza kushuhudia tukio hilo kubwa duniani la kutangazwa kwa kwa raia
huyo wa Albania ambaye alifariki mwaka wa 1997.
Mama Tereza alianzisha
shirika la hisani la kimishenari ili kuwasaidia walala hoi katika mtaa wa
mabanda wa Calcutta nchini India.
Lakini wakosoaji wanesema
kuwa Mama Teresa hakuwasaidia watu waliokuwa wagonjwa na alilaumiwa kwa
kujaribu kuwabadilisha dini watu maskini wa kabila la Hindu nchini India kuwa
Wakristo.
Sherehe za kutangazwa kuwa
mtakatifu kwa mshindi huyo wa tuzo ya amani ya Nobel, zimehudhuriwa na wageni
zaidi ya 1,000 wakiwemo wakuu wa nchi mbalimbali 13 na viongozi wa madhehebu
hayo.
Ulinzi umeimarishwa wakati
wa sherehe hizo. Mama Teresa aliyezaliwa mwaka 1910 katika taifa ambalo hivi
sasa linajulikana kama Macedonia, alianza huduma ya utawa akiwa na umri wa
miaka 16.
Ilikuwa ni kazi yake ya
kuwasaidia wagonjwa na maskini huko Calcuta, India iliyompatia umaarufu mkubwa
duniani kote, pamoja na kupokea tuzo ya amani ya Nobel.
Papa Francis amesema huruma
aliyokuwa nayo Mama Teresa inapaswa kuwa mfano kwa Wakatoliki wote. Kutawazwa
kwa mtawa huyo kunakuja miaka 19 baada ya kifo chake.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...