Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi ya Ardhi Tanzania, Dr. Stephen Nindi akizungumza jambo juu ya Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa pamoja kuhakikisha maeneo yanapimwa na kuweka mpango mzuri wa Matumizi Bora ya Ardhi.
Mkutano ukiendelea
Katika kupanga matumizi bora ya ardhi nchini Tanzania ikiwa na lengo la jamii kutumia rasilimali hiyo vizuri kwa matumizi ya kawaida, Serikali imesema kuwa hadi sasa imefikia takribani vijiji 1645 na Wilaya 40 nchi nzima. Kutokana na ufinyu wa bajeti na kasi ndogo ya upimaji bado kuna vijiji 11,393 ambavyo havijafikiwa.
Akizungumza Mkoani Morogoro ,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Ardhi,Dkt Stephen Nindi wakati wa Mkutano wa Kikosi kazi cha kuanda mpango kazi wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa maendeleo ya Ardhi nchini.
Pia Mkutano huo ulijadili kuhusu migogoro ya ardhi inayoendelea nchini na mipango ya matumizi ya ardhi kama inaweza kusaidia kupunguza migogoro hiyo,uliowakutanisha wadau mbalimbali kutoka Serikalini ,taasisi na Mashirika mbalimbali yanayosimamia masuala ya ardhi.
Alisema serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanashirikiana kwa pamoja kuhakikisha maeneo yanapimwa na kuweka mpango mzuri wa matumizi ya ardhi kwa matumizi yaliyokusudiwa katika kujadiliana ni namna gani wataona njia zinazofaa kutumika kukamilisha zoezi hilo la upimaji kwa vijiji vingine ikiwemo kuwepo kwa teknolojia mpya ya upimaji na kuwepo kwa bajeti ya kutosha.
Aliongeza kuwa lengo la kupima,kumilikisha na Kupanga kila kipande cha ardhi ni pamoja na kuhakikisha ardhi inakuwa na matumizi mazuri katika nchi.
Dkt.Nindi alisema tayari serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wametoa elimu katika timu za wilaya 100 kuwawezesha kujua kupima,kupanga,kumilikisha ,kutekeleza na kusimamia mipango ya matumizi ya ardhi .
Kwa upande wake Mratibu wa Programu ya Mradi ya Ardhi yetu kutoka Shirika la Kimataifa la CARE nchini Tanzania ,Mary Ndaro alisema mpaka sasa ni miaka mingi tangu nchi ipate uhuru kasi ya upimaji wa maeneo imekua ndogo .
Alisema kama nchi inajiandaa kuwa na wawekezaji wengi zaidi inatakiwa kuhakikisha inakuwa na mipango bora ya matumizi ya ardhi ambayo baadae haitaweza kuleta mgogoro wowote kati ya wanakijiji na muwekezaji.Aliongeza kuwa kwa sasa kati ya vijiji 12,545 nchi nzima ni vijiji 1645 ndiyo tayari vina mipango ya matumizi ya ardhi mpaka sasa.
Vijiji vingi bado havina mipango kutokana na ufinyu wa bajeti na kuwepo kwa kasi ndogo ya upangaji.Ndaro alisema lengo la mkutano huo wa wadau ni kuona ni namna gani vijiji vilivyobaki kati ya vijiji 12,545 vinapangiwa matumizi ya ardhi, kunakuwa na ushirikiano wa karibu wa wadau na namna vipi wanashirikiana kutatua migogoro ya ardhi ambayo inazidi kuongezeka.
Vijiji vingi bado havina mipango kutokana na ufinyu wa bajeti na kuwepo kwa kasi ndogo ya upangaji.Ndaro alisema lengo la mkutano huo wa wadau ni kuona ni namna gani vijiji vilivyobaki kati ya vijiji 12,545 vinapangiwa matumizi ya ardhi, kunakuwa na ushirikiano wa karibu wa wadau na namna vipi wanashirikiana kutatua migogoro ya ardhi ambayo inazidi kuongezeka.
“Pamoja na kuwepo kwa kasi ndogo ya upangaji matumizi ya ardhi, bado kuna changamoto ya kutoheshimu mipango ya matumizi ya ardhi iliyokwishaandaliwa ambapo utakuta kijiji tayari kimepangwa lakini kinakuja kukatwa katikati na kuwa vijiji viwili au zaidi,”alisema
Alisema serikali inapaswa kuweka mipango ya matumizi ya ardhi ipasavyo ili kuweza kudhibiti hali ya migogoro ya ardhi kati ya watumiaji mbalimbali, mfano baina ya wawekezaji na wanavijiji kwa kupanga matumizi ya ardhi.“Serikali inapoita wawekezaji nchini inapaswa pia kuhakikisha mpango ya matumizi bora ya ardhi inayoeleweka kwa lengo la manufaa ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla,”alisema
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...