Pichani kulia ni Kaimu katibu mkuu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) Taifa ,Shaka Hamdu Shaka akiongea na waandishi wa habari mjini Dodoma,shoto ni kaimu katibu wa hamasa,sera,utafiti na mawasiliano wa UVCCM Taifa Chief Silvester Yeredi

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema  hakuna mazungumzo, majadiliano wala mijadala inayostahili kufanyika kati ya Serikali ya CCM na Chadema na kuiomba Serikali ya Rais Dk John Magufuli iendelee na mikakati yake ya kisera ili kuimarisha maendeleo ya kiuchumi.

Pia umoja huo  umeeleza kuwa  dunia inajua, ulimwengu unaaelewa na Chadema wanafahamu kuwa Tanzania hakuna mgogoro wa kisasa zaidi ya serikali kupigania mabadiliko, nchi kuwa ya viwanda na kutokomeza  maadui umasikini, ujinga na maradhi.

Msimamo huo umetolewa jana na Kaimu Katibu Mluu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka, katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika ukumbi wa White House Makao Makuu ya CCM Mkoani hapa.

Shaka alisema UVCCM ilijua, ilielewa na kutambua mapema  Chadema na viongozi wake walikuwa wakifanya maigizo katika  siasa, hawakuwa na ubavu wala jeuri ya kuandamana kwa madai aliyoyaita ni ya  kipuuzi ambayo hayana msingi kwa mustakabali wa nchi na maendeleo yake.

Alisema viongozi na wafuasi wa Chadema  walishindwa kuandamana Septemba Mosi, hawataweza na wala hawatajaribu kufanya hivyo  Oktoba Mosi kwa sababu wanachotaka kukifanya ni utoto wa kisiasa  baada ya kushindwa kubuni mkakati wa kukiendesha chama chao ili kiaminike na kukubalika.

"Tunazo habari  wabunge wa Chadema wamechachamaa na kumbana Mbowe  kwa  hoja wakitaka kurudi bungeni ili kushiriki vikao kwa kuwa hawaeleweki kwa wapiga kura wao majimboni lakini pia wanakabaliwa na 'waya mkali',   hawaoni kwa nini wasishiriki vikao vya Bunge huku baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho wakiwa na utajiri na wengine  wafanyabiashara,"alisema Shaka.

"Cha ajabu hata na wale wazee tuliokuwa tukiwaheshimu bila soni wanashiriki kuudanganya ulimwengu wakitoa madai ati kuna mgogoro wa kisiasa  unaohitaji suluhu, yafanyike mazungumzo na majadiliano,"alisema Shaka.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...