Kipa wa Timu ya Azam FC "Wanalambalamba", Aeshi Manula akiwa chini huku Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akijiandaa kushangilia baada ya Kipa huyo kupitwa na mpira uliopigwa vizuri kabisa na Mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya (hayupo pichani) na kuingia moja kwa moja wavuni na kuifanya timu hiyo kujipatia bao la kuongoza. Mchezo huo ambao ulikuwa ni wenye kasi na wakuvutia huku timu zote zikishambuliana kwa zamu, umemalizika jioni hii kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam huku Timu ya Simba ikiondoka uwanjani hapo ikiwa kifua mbele kwa ushindi wa bao 1-0. Kwa ushindi huu wa leo, Timu ya Simba sasa inashikilia ushukani wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ikiwa na pointi 13, ikifuatiwa na mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 10 sawa na Azam FC.
 Mshambuliaji wa Timu ya Azam FC, John Bocco akituliza Mpira mbele ya Beki wa Simba, Novaty Lufunga, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshida bao 1-0.
 Beki wa Azam FC, David Mwantika akindoka na mpira baada ya kumshinda maarifa, Mshambuliaji wa Simba, Fredrick Blagnon, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshida bao 1-0.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...