Kipa
wa Timu ya Azam FC "Wanalambalamba", Aeshi Manula akiwa chini huku
Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo akijiandaa kushangilia baada ya
Kipa huyo kupitwa na mpira uliopigwa vizuri kabisa na Mshambuliaji wa
Simba, Shiza Kichuya (hayupo pichani) na kuingia moja kwa moja wavuni na
kuifanya timu hiyo kujipatia bao la kuongoza. Mchezo huo ambao ulikuwa
ni wenye kasi na wakuvutia huku timu zote zikishambuliana kwa zamu,
umemalizika jioni hii kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam huku
Timu ya Simba ikiondoka uwanjani hapo ikiwa kifua mbele kwa ushindi wa
bao 1-0. Kwa ushindi huu wa leo, Timu ya Simba sasa inashikilia ushukani
wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ikiwa na pointi 13, ikifuatiwa na mabingwa
watetezi, Yanga SC wenye pointi 10 sawa na Azam FC.
Mshambuliaji
wa Timu ya Azam FC, John Bocco akituliza Mpira mbele ya Beki wa Simba,
Novaty Lufunga, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni
ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshida bao
1-0.
Beki
wa Azam FC, David Mwantika akindoka na mpira baada ya kumshinda
maarifa, Mshambuliaji wa Simba, Fredrick Blagnon, katika Mchezo wa Ligi
Kuu Tanzania Bara, uliopigwa jioni ya leo kwenye
Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. Simba imeshida bao 1-0.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...