Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Bi. Sarah Kibonde Msika akitoa maelezo na kugawa vijarida kuhusu hifadhi ya Jamii kwa baadhi ya wageni waliotembelea banda la SSRA katika maonesho ya Wiki ya Fedha, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Afisa wa SSRA, Bi. Amina Ally akitoa mada katika Semina ya uhamasishaji wa Hifadhi ya Jamii kwa wajasiriamali wadogo walioshiriki katika mafunzo yaliyokuwa yakitolewa katika Wiki ya Fedha yaliyofanyika viwanja vya Mnazi Mmoja hivi karibuni.
Maofisa wa Mamlaka, Bi. Imani Masebu (kushoto) na Bi. Agnes Lubuva (kulia) wakitoa maelezo kuhusu umuhimu wa Hifadhi ya Jamii kwa wajasiriamali wadogo waliotembelea banda la SSRA katika maonesho ya wiki ya Fedha hivi karibuni.
Afisa wa Mamlaka Bw. Athumani Juma akigawa vipeperushi na vijarida vya uhamasishaji wa umuhimu wa kujiunga na Hifadhi ya Jamii kwa wajasiriamali wadogo waliotembelea banda la SSRA katika maonesho hayo, hivi karibuni.
Afisa wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Ally Masaninga akitoa maelezo kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa na Mamlaka pamoja na kugawa vipeperushi kwa washiriki waliotembelea Banda la SSRA katika maonesho ya wiki ya Fedha, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kushoto), katika meza kuu akiwa na viongozi wa maonesho ya wiki ya Fedha pamoja na wawakilishi wa Mashirika na Taasisi mbalimbali ikiwemo SSRA, wakifuatilia kwa makini risala toka kwa wajasiriamali (hawapo pichani), katika siku ya kilele cha maonesho ya Fedha, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...