TETEMEKO: MALINZI AWAPA POLE KANDA YA ZIWA, BURUNDI NA UGANDA

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameshitushwa na taarifa za tukio la tetemeko kubwa ardhi lenye mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 lililotokea jana Septemba 10, 2016 katika mikoa mitatu ya Kanda ya Ziwa kadhalika nchi za Burundi na Uganda.

Mikoa ya Kanda ya Ziwa iliyopata athari kwa mujibu wa taarifa ni Mwanza, Mara na Kagera nchini na kuripotiwa kuua zaidi ya watu 10 na wengine zaidi ya 120 kujeruhiwa sambamba na kubomoa majengo mbalimbali.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini 


AFRICAN LYON V MBAO FC

African Lyon ya Dar es Salaam kesho Septemba 12, 2016 itaikaribisha Mbao FC kwenye mchezo Mchezo huo Na. 28 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara utakaofanyika Uwanja wa Uhuru jijini. Mara baada ya mechi hiyo, raundi ya tano itafanyika mwishoni mwa wiki ijayo kadiri ya ratiba.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini


ZIARA YA NAPE NA RIPOTI KAMILI YA TFF

Ripoti ya mwenendo wa mpira wa miguu Tanzania na mipango yake inayofanywa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imemfurahisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye hivyo moja kwa moja akaupongeza uongozi wa Rais Jamal Malinzi akisema unafanya kazi kubwa.

Kutokana na ripoti hiyo, Nape ambaye ni Mbunge wa Mtama mkoani Lindi, aliridhia wadau wa mpira wa miguu kusapoti timu za taifa hususani Serengeti Boys – timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ambayo kwa sasa imepiga kambi Shelisheli kujiandaa kuivaa Congo-Brazzaville Jumapili ijayo.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini


MALINZI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA SIANG’A

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea taarifa za kifo Kocha wa zamani wa Simba, James Aggrey Siang’a. Taarifa kutoka Kenya zinasema amefariki leo Septemba 10, 2016 alfajiri mjini Bungoma baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Siang’a alikuwa ni miongoni mwa makocha walioheshimika Afrika Mashariki hususani Tanzania alipoingoza Simba kufanya vema kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kufika hatua ya timu Nane Bora.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...