Meneja Mwandamizi wa Usambazaji Umeme wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), ambaye pia ndiye Meneja wa Mradi wa kuimarisha miundombinu ya Umeme, Injinia Theodory Bayona.(katikati), akisimamia kazi hiyo leo Septemba 3, 2016.

NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID
WAHANDISI, na mafundi wa Shirika la Umeme Nchini Tanzania, (TANESCO), kwa kushirikia na wale wa kampuni za Kijapani za Yachiyo Engineering Co Limited, Takaoka na National Construction Co. Limited, wameanza kazi ya uboreshaji miundombinu ya umeme kwenye kituo kikubwa cha kupooza na kusambaza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam, imeanza leo Septemba 3, 2016.

Kazi kubwa inayofanyika hivi sasa ni kubadilisha laini kutoka umeme mdogo kwenda umeme mkubwa, lakini pia kubadilisha vifaa vingine muhimu ili kuwezesha usafirishaji umeme uweze kuwafikia watumiaji katika ubora ulio juu.

“Ikumbukwe kwamba, hapa tulikuwa na laini mbili (waya mbili) zilizokuwa na uwezo wa kusafirisha umeme kiasi cha Megawati 120 kila moja, kutoka hapa Ubungo kwenda kituo cha Ilala, lakini kazi inayofanyika sasa, ni kubadili njia hizo (waya za umeme), ambazo zitakuwa na uwezo wa kupitisha kiasi cha umeme wenye Megawati 220 kila moja,” Alifafanua Meneja Muandamizi wa Usambazaji Umeme wa Shirika hilo, ambaye pia ndiye Meneja wa wa Mradi wa kuimarisha miundombinu ya Umeme, Injinia Theodory Bayona.

Kwa mantiki hiyo, kazi inayofanyika leo hii itawezesha umeme utakaokuwa ukisafirishwa kutoka hapa Ubungo kwenda Ilala, kuwa na jumla ya Megawati 440 kwa laini zote mbili, tofauti na hapo awali ambapo uwezo wa kusafirisha umeme ulikuwa Megawati 240 tu,” Alisema.

Kazi ikikamilika wakazi wa jiji la Dar es Salaam, watakuwa wakipata umeme wa uhakika, na ulio bora, alifafanua Injinia Bayona.

Naye Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Nchini Tanzania, (TANESCO), Leila Muhaji, amewaomba wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambapo Shirika linafanya juhudi kubwa za kuwapatia umeme wa uhakika wananchi kwa kuimarisha miundombinu yake,.

“Ili kuwawezesha mafundi wetu kufanya kazi katika mazingira salama, tutakuwa tukikata umeme kuanzia leo hii Septemba 3 na umeme utakuwa ukikatika kuanzia saa 2 asubuhi na kurejea saa 11 jioni kwa utaratibu na tarehe kama ifuatavyo; Septemba 3-4, Septemba 10-11, Septemba 17-18, na Septemba 24-25, 2016.” Alifafanua Leila, na kuwaomba wananc hi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki.

Mradi huu ulioanza Februari 2015 na unaotarajiwa kukamilika Juni 2017 unatekelezwa na Serikali kupitia TANESCO kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA).
Fundi wa TANESCO, akifunga kikombe wakati wa kazi ya kubadilisha miundombinu ya kusafirisha umeme kwenye kituo kikuu cha kupooza na kusambaza umeme cha Ubungo, jijini Dar es Salaam
Raphael Mjata, Msimamizi Mkuu wa Njia Kuu za Umeme, akionyesha uwezo wa kituo cha Ubungo cha kupooza umeme wenye kilovolti 132.
Mafundi wa TANESCO na kampuni ya National Construction Company Limited, wakivuta nyaya hizo mpya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...