Mwenyekiti wa Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss), Anna Matinde akizungumza katika hafla ya kutimiza Miaka miwili ya TASWE-Saccos jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 

Alisema kuwa TASWE ipo mikoa Tofautitofauti hapa nchini Lengo kuu la hafla ya Dinner Part Gala ni kuwafikia wanawake wengi zaidi ili kutatua changamaoto zinazowakabiri hasa kwa upande wa kipato cha mwanamke.

Alisema kuwa TASWE inamatawi 14, katika matawi hayo wameona watoe elimu ya Ujasiliamali kwa wanawake wengi zaidi hapa nchini ili kupunguza ongezeko la utegemezi na waweze kuwa wanawake wajasili na wenye nguvu.
 Rais wa Chama cha wenye viwanda Biashara na Kilimo nchini (TCCIA), John Mayanja akizungumza wakati wa kuadhimisha miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kuwataka wanawake watumie fursa zinazojitokeza hasa kwa wale wanaotaka kusindika juisi za matunda hapa nchini kwa kuwa kuna matunda mbalimbali inapofikia msimu wake huharibika na kutupwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Plc, Ineke Bussemaker, akizungumza na wanawake wakati wa kusheherekea Miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) tangu kuazishwa kwake na kuwa na wanachama wanawake wengi katika mikoa tofauti tofauti zaidi ya 10 hapa nchini. Alisema kuwa Wanawake milango imefunguka kwa benki hiyo hasa wakijiunga kwa makundi ili kupata mikopo yenye riba ya chini katika benki ya NMB hapa nchini.
 Wanawake wakiserebuka wakati wa kusherekea miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Rais wa Chama cha wenye viwanda Biashara na Kilimo nchini (TCCIA), John Mayanja atembelea baadhi ya kazi za wanawake wajasiliamali katika hafla ya Dinner Paty Gala iliyoambatana na Kusheherekea miaka miwili ya Tanzania Saccos For Women Entrepreneurs (TASWE - Saccoss) jijini Dar es Salaam.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...