Na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Bukoba.
Shirika la Kiristo la Kuhudumia
Wakimbizi Tanganyika (TCRS) limechangia vifaa vyenye jumla ya Sh. milioni 60.92
ikiwa ni mchango wao wa kuwafuta machozi wanakagera baada ya kuathiriwa na
tetemeko la ardhi.
Katika kuhakikisha hali za wananchi
na ttaasisi za kutolea huduma za kijamii zinaimarika na kurudi
kwenye hali ya kawaida, wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi bado michango
yao inahitajika.
Akikabidhi mchango huo, Mratibu wa
Miradi inayoendeshwa na TCRS Oscar Rutenge pamoja na Jasmine Gwamsy wametaja
mchanganuo wa msaada huo kuwa ni pamoja na blanketi, 1680, mashuka 840, ndoo za
kutumia 840, nguo za kutumia kwawanawake, wanaume na watoto box 50, sabuni
katoni 1680 pamoja na vifaa vingine 2250.
Akipokea msaada huo Mkuu wa Mkoa wa
Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu amemelishukuru shirika hilo kwa
mchango wao huo kwani ni wa thamani hasa baada ya tetemeko hilo kuwaaathiri
wananchi wa mkoa huo.
Aidha, Meja Jenerali Mstaafu Kijuu
amewakaribisha na kuwataka wadau wengine waguswe kwa namna ya kipekee na
waendelee kutoa michango yao waweze kuwasaidia wananchi na kurudisha hali yao na
kuendelea na shughuli zao za kijamii na kimaendeleo.
Mkuu wa msafara wa Shirika la Kiristo la
Kuhudumia Wakimbizi Tanganyika (TCRS) Jasmine Gwamsy akimkabidhi Mkuu wa Mkoa
wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu vifaa vyenye thamani ya jumla ya
Sh. milioni 60.92 ikiwa ni mchango wao wa kuwafuta machozi wanakagera baada ya
kuathiriwa na tetemeko la ardhi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...