Kufuatia hali inayoukabili mkoa wa Kagera kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo mnamo septemba 10 mwaka huu na kusababisha maafa makubwa kwa baadhi ya Wananchi na hata kuchukua uhai wa watu 17 Mkoani humo
Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania (TPDC) limeungana na jitihada za Serikali katika kusadia waathirika wa tetemeko Mkoani humo kwa kutoa  vifaa vya ujenzi ikiwa ni pamoja na saruji na mabati vyenye thamani ya shilingi millioni 20 kwa ajili ya kusaidia ujenzi kwa walioguswa na maafa hayo.
Baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji TPDC Mhandisi, Kapuulya Musomba amesema kuwa wametoa vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi millioni 20 kwa ajili ya kuwasadia waathirika wa tetemeko hilo.
Pia Mhandisi Musomba amesema kuwa misaada waliotoa sio mwisho badala yake watahakikisha wanaendelea kuwafuatilia kampuni washirika wanaofanya kazi na TPDC nchini, huku akiongeza kuwa tayari wameshawaandikia barua ya kuwaomba kuchangia na kushiriki katika kusaidia Wanakagera.
 Kaimu Mkurugenzi wa TPDC Mhandisi, Kapuulya Musomba akipeana  mikono na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya kukabidhi msaada wa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni ishirini (20,000,000) kwa waathirika wa tetemeko Mkoani Kagera.
 Mjumbe wa Bodi ya TPDC Balozi Ben Moses akikabidhi nyaraka zenye orodha ya vifaa vya ujenzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu vilivyo kabidhiwa na TPDC.
Zoezi la kukabidhi misaada iliyotolewa na TPDC kwa waathirika watetemeko Mkoani Kagera likiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...