.Mkurugenzi wa Uhamasishaji Sera na Utafiti wa TPSF,Gili Teri akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wakujadili Agenda maalum inayohusisha masuala mbalimbali yakiwemo ya Kilimo,Nishati,Elimu na mengineyo.
.Baadhi ya Wadau wa Sekta Binafsi na Wafanyabiashara wakiwa katika semina hiyo.

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini(TPSF) imekutana na Wafanyabiashara pamoja na wadau wa Sekta Binafsi ili kutengeneza Agenda ya Biashara ya Taifa.

Agenda hiyo ina lengo la kukusanya maoni pamoja na matarajio ya wadau wa Sekta Binafsi hususan kuelekea katika Uchumi wa Viwanda miaka 5 na 10 ijayo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika semina maalum iliyowakutanisha Wadau wa Sekta Binafsi,Mkurugenzi wa Uhamasishaji Sera na Utafiti wa TPSF,Gili Teri amesema Agenda hiyo inahusisha masuala mtambuka lakini masuala halisi ya Kisekta yakiwemo ya Kilimo,Nishati,Elimu na Sekta nyingine mbalimbali.

"Mazingira ya Biashara yanapoboreshwa mimi na wewe tunaofanya biashara tunaweza kufaidika zaidi,tukaajiri watu wengi na tukalipa kodi zaidi,"amesema Teri

Amesema wanatengeneza agenda ya pamoja ambayo itatumika kama kitu cha ambacho kitaongoza mawasiliano kati ya Sekta Binafsi pamoja na wadau wengine wakiwemo Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...