Na Anthony John, Globu ya jamii.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanahabari,Theophil Makunga ameipongeza Serikali kwa niaba ya wanahabari kwa kuanza mchakato kuondoa Sheria ya Magazeti ya mwaka1976 kwani Sheria hiyo amedai ilikuwa inawabana wanahabari. Pia akifafanua kuwa,serikali imeanza mchakato wa kubadilisha Sheria  hiyo ya Magazeti iliyo kuwepo kwa Miaka 40 tangu ianze kutumika,hivyo alisema Sheria itakayo anzishwa itafanya kazi kwa muda mrefu kwa Miaka 40 hadi 50.
Serikali imesikiliza kilio cha wanahabari na imeanza mchakato wa kubadilisha hiyo Sheria,sasa kwa sababu hiyo kama alivyosema katibu ni kwamba Sheria hiyo imekaa kwa muda wa Miaka 40 kwa hivyo hata mpya itakayotugwa sasa itakaa Miaka 40 hadi 50 inayokuja.
Hivyo Hivyo,Katibu Mkuu wa Jukwaa la wanahabari Neville Meena amesema watapata maoni ya wadau mbali mbali wa Habari kupitia klabu za waandishi wa habari watakao kwenda kuwaeleza maudhui yaliyomo ndani ya Sheria yenyewe ilikupata maoni yao wenyewe vila kuwashawishi.
"Maana yake tukienda kufanya uchambuzi watachukua maoni yetu kama maoni yao, hata hivyo tumekuwa tukipokea lawama nyingi kutoka kwa waandishi kutokushiriki na wakati wao ndio wako kwenye vyombo vya Habari" hayo,"amesema  Meena. 
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanahabari Bw. Theophil Makunga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya kuipongeza Serikali kwa niaba ya wanahabari kwa kuanza mchakato wa kuondoa Sheria ya Magazeti ya mwaka1976 kwani Sheria hiyo ilikuwa inawabana wanahabari leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wanahabari, Bw. Neville Meena.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...