Image result for kuku wa mayai na nyama
Na Woinde Shizza, Arusha.

Wajasiriamali nchini wametakiwa kujikita katika Ufugaji wa kuku wa Kienyeji na kisasa ili waweze kunufaika kiuchumi kufuatia ongezeko la uhitaji mkubwa wa mayai na nyama katika maeneo ya mengi hususan kwa wafanyabiashara wa vyakula.

Hayo yameelezwa na Mjasiriamali Boniventura Shiyo anayejihusisha na ufugaji huo kuwa kwa sasa biashara hiyo imemuongezea kipato ambacho anakitumia kujiletea maendeleo pamoja na kuendesha familia pasipo kuyumba.

Mjasiriamali huyo amewataka Watanzania kujenga tabia ya uthubutu kwani soko la biashara ya kuku ni kubwa na linazidi kukua kila kukicha.

Hata hivyo Boniventura amesema kuwa kwa sasa anatumuia mashine maalumu ya inayototoa mayai na kuwa vifaranga maarufu kama incubator ambayo imemuongezea fursa ya kuwa muuzaji wa vifaranga pia.

Biashara ya ufugaji wa kuku ni moja kati ya biashara zinazoshamiri kwa kasi katika maeneo mingi nchini hususan maeneo ya mijini ambapo ndipo masoko makubwa yanapatikana kutokana na idadi kubwa ya watumiaji wa bidhaa za mayai na nyama ya kuku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...