Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk Binilith Mahenge amefanya ukaguzi wa zoezi la ununuzi wa mahindi msimu wa 2016/2017.Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula(NFRA) lands ya Songea umepanga kununua tani 20,000 za mahindi toka kwa wakulima .
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dk.Binilith Mahenge akiongea na wakulima (hawapo pichani) kwenye kituo cha ununuzi mahindi kijiji cha Rwinga wilaya ya Namtumbo.Kushoto ni mkurugezi wa Uendeshaji toka NFRA Nicodemus Masawe na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Luckiness Amlima.
Mahindi ya wakulima wa kijiji cha Mgazini wilaya ya Songea yakiwa kwenye kituo cha ununuzi.Zoezi la kununua mahindi limeanza ambapo kilo moja ya mahindi inanunuliwa shilingi 510.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...