Balozi wa Japan Nchini, Masaharu Yoshida, akionyesha sehemu ya msaada uliotolewa na Serikali ya Japan  leo jijini Dar es Salaam, ukishuhudiwa na  Katibu  Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Projest Rwegasira.
Katibu  Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Projest Rwegasira  akizungumza na waandishi wa habari wa kupokea msaada wa dola  za kimarekani milioni 1.8 kwa ajili ya kununulia chakula cha wakimbizi zaidi ya 200,000  ambapo msaada huo unakwenda shirika la lisilo la serikali leo jijini Dar es Salaam.

Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii.
WAKIMBIZI zaidi 200,000 walio katika Mikoa ya Kasikazini na Magharibi nchini wapwa msaada wa chakula kilichogharimu Dola za Marekani Milioni  1.8 kutoka serikali ya Japan.

Msaada huo umeshudiwa na Katibu  Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali, Projest Rwegasira wakati wa mkabidhiano ya msaada kutoka kwa Balozi wa Japan Nchini, Masaharu Yoshida, pamoja na Mwakilishi Mkazi wa WFP nchini Tanzania.

Balozi wa Japan amesema kuwa msaada huo kwa serikali ya Tanzania  ni wa kiubinadamu wa kukubali kuwa na wakimbizi.
"Serikali ya Japan imefurahishwa na utoaji wa fedha hizo kwa ajili ya msaada wa chakula kwa wakimbizi walioko nchini Tanzania kutokana na wakimbizi kukosa chakula na hali ya duni ya lishe." 

Kwa juhudi ambazo zinafanywa ni kutaka kuboresha upatikanaji wa chakula kwa maisha ya wakimbizi waendelee kukaa kwa amani katika mikoa ya kaskazini na magharibi mwa Tanzania.

Amesema fedha hizo  ni sawa na bidhaa tani 1,800 ambazo zimetolewa na serikali ya Japan ikiwa ni virutubishi vya mafuta, pamoja na tani za mahindi 1,100 pia manunuzi ya vyakula vya virutubishi vya uji kwa ajili ya wakina mama na watoto walio katika hatari ya kupata utapiamlo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...