MKURUGENZI
Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel amesema
wanafunzi wanaokwenda nje waliohitimu masomo katika vyuo vya nje
wanatakiwa watafutwe na waajiri na sio wawe wa kutafuta ajira.
Mollel ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa semina na wazazi na wanafunzi 200 wanaotarajia kuondoka kesho katika vyuo vikuu vya nchini China, amesema kuwa kutokana na vyuo hivyo kuwa na vifaa vya kujifunzia wanafunzi wakitumia vizuri katika soko la ajira watatafutwa.
Mollel amesema nchi haina tatizo la ajira hivyo watu wanatakiwa kuwa na uwezo binafsi ambao utamfanya mwajiri kutafuta mtu wa kumuajiri hivyo wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo wanatakiwa kutumia maarifa ya kuja kuzalisha nchini.
Amesema wazazi watumie muda wao katika kuwafuatilia watoto wao wanaosoma nje ili kuweza kuona thamani ya fedha wanazozitoa na elimu wanayoipata.
Aidha amesema kuwa wale ambao wanahitaji vyuo vya nje bado nafasi zipo na wanafunzi wote watafuata taratibu zote ikiwa ni pamoja Tume ya Vyuo Vikuu nchini kujiridhisha na vyuo wanavyokwenda. Mollel amesema haitakuwa tayari kuona wanafunzi wanahitimu vyuo vya nje kupitia GEL kuwa hawatambuliki.
Mollel ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa semina na wazazi na wanafunzi 200 wanaotarajia kuondoka kesho katika vyuo vikuu vya nchini China, amesema kuwa kutokana na vyuo hivyo kuwa na vifaa vya kujifunzia wanafunzi wakitumia vizuri katika soko la ajira watatafutwa.
Mollel amesema nchi haina tatizo la ajira hivyo watu wanatakiwa kuwa na uwezo binafsi ambao utamfanya mwajiri kutafuta mtu wa kumuajiri hivyo wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo wanatakiwa kutumia maarifa ya kuja kuzalisha nchini.
Amesema wazazi watumie muda wao katika kuwafuatilia watoto wao wanaosoma nje ili kuweza kuona thamani ya fedha wanazozitoa na elimu wanayoipata.
Aidha amesema kuwa wale ambao wanahitaji vyuo vya nje bado nafasi zipo na wanafunzi wote watafuata taratibu zote ikiwa ni pamoja Tume ya Vyuo Vikuu nchini kujiridhisha na vyuo wanavyokwenda. Mollel amesema haitakuwa tayari kuona wanafunzi wanahitimu vyuo vya nje kupitia GEL kuwa hawatambuliki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel akizungumza katika semina ya wazazi na wanafunzi 200 wanaotarajia kuondoka kesho kwenda vyuo vikuu vya nchini China, iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wanaokwenda nje wakichukua tiketi pamoja na viza kwa ajili ya safari kwenda katika vyuo vikuu vya nchini China iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wazazi na wanafunzi wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel hayupo pichani katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...