Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe Akifurahia wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya kuzungumza nao jambo alikutana nao waliokuwa walipomaliza kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni mkoani Tanga.

Wanafunzi hao wamemwambia Mkuu wa wilaya Mh. Godwin Gondwe kufikisha salamu zao kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli, wakimshukuru kwa kuwezesha elimu ya Msingi mpaka Sekondari kuwa bure , kwani itarahisha wanafunzi wengi ambao wazazi wao hawana uwezo kupata elimu. Wameongeza kuwa "Mtihani ulikuwa mzuri hivyo watafauru kwa kishindo".
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe Akipiga picha ya pamoja na wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya wanafunzi hao kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni.
Wanafunzi wa shule ya Msingi Chanika wilayani Handeni wakifurahia jambo mara baada ya kumaliza elimu ya Msingi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...