Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nandi Mwiyombella (kulia) akishuhudia mojawapo ya mechi za Vodacom Premier League katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam hivi karibuni. |
Wadhamini
wakuu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara , “Vodacom Premier League” imesikia
kilio cha mashabiki na wapenzi wa soka nchini na kuamua kuwaletea kifurushi
maalumu kinachojulikana kama ‘Soka bando’ ambacho ni mahususi kwa ajili ya
mashabiki wa mchezo wa mpira wa miguu unaopendwa duniani kote.
Vodacom
Tanzania imebuni kifurushi hiki kwa ajili ya kuwapatia taarifa za soka za hapa
nchini na ligi za kimataifa kwa gharama nafuu ya shilingi 500/-Kifurushi cha
‘Soka bando’ kitakuwa kinawapatia mashabiki wa soka muda wa maongezi wa dakika
14 Vodacom kwenda Vodacom na pia dakika 2 vodacom kwenda mitandao mingine, na
pia utapata sms 20 kwa saa 24.
Mkuu
wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nandi Mwiyombella amesema
“Kwa gharama nafuu ya shilingi 500/-mashabiki wa soka wanaotumia mtandao wa
Vodacom watapata taarifa mbalimbali za soka za hapa nyumbani na kimataifa
kwa kipindi cha siku 7,dakika 14 za muda wa maongezi Vodacom kwenda Vodacom,
dakika 2 za muda wa maongezi kwa mitandao yote na jumbe fupi za maneno
(SMS) 20 kwa kipindi cha masaa 24”
Alisema
Vodacom Tanzania imeleta kifurushi hiki cha ‘Soka bando’ kipindi hiki ambacho
msimu wa ligi ya VPL unaendelea ni furaha kwa Mtandao wa Vodacom kuwawezesha
mashabiki kupata taarifa za ligi kwa urahisi kupitia mtandao wake ikiwemo
kuwapatia burudani wateja wake na watanzania wote kwa ujumla.
“Kampuni
inathamini na kutambua mchango wa mashabiki katika kukuza ligi hii tangu
ilipoanza kuidhamini hivyo ndio maana tumewaletea kifurushi hiki ili
wapate burudani na taarifa za soka kwa wakati na kwa gharama
nafuu”.Alisema Mwiyombella.
Ili
kununua kifurushi hiki anachotakiwa kufanya mteja ni kupiga namba *149 *
01#, na kuchagua ‘Soka Bando’. Baada ya hapo mteja atapata ujumbe
unaomtaka ajisajili kwa timu ya soka anayoishabikia kwa kutuma jina la timu mfano
“Yanga” “Simba” au “Azam” nk. kwenda namba 15460.Pia mteja anaweza kupata
taarifa za soka kupitia tovuti ya Mspoti.vodacom.co.tz.
Wateja
watakaojiunga na huduma hii pia watapata nafasi ya kufurahia ofa na
zawadi mbalimbali kutoka Vodacom kama vile muda wa bure wa maongezi, sms
au MB za akuperuzi inteneti hususani timu wanazoshabikia zitakapokuwa
zimeibuka na ushindi wa mchezo.
Msimu
mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara unaendelea katika viwanja
mbalimbali nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...