Watanzania waishio eneo la Bay area- Northen California, jana kwa pamoja walikusanyika katika kanisa la Lutheran Oakland ili kukusanya michango ya waathirika wa tetemeko la ardhi lilitokea kanda ya ziwa nchini Tanzania, hususan mkoani Kagera ambako madhara makubwa yamerekodiwa.
 Jumla ya dola za Kimarekani  4,000 za ahadi na fedha taslim zilipatikana hiyo jana.
“Tuna mpango wa kukusanya pesa zote   ifikapo Jumamosi  Septemba 24, 2016 na kuzituma  Jumatatu Septemba  26, 2016 katika  ofisi ya Mkuu wa mkoa  wa Kagera ambapo shughuli zote uratibu na makusanyo yote yanaelekezwa pale kama serikali ilivyoagiza” amesema Bw.
Erick Byorwango, Katibu mwenezi wa Jumuiya ya Watanzania - Northern California. 
 Bw. Byorwango ameongeza kusema kuwa jitihada za kukusanya michango zinaendelea na mwitikio wa mkutano huu ulikuwa na matumaini. 
"Tunaomba mungu aendelee kutupa nguvu na upendo ili tukamilishe zoezi hili na hatimaye tuwakilishe msaada wetu serikalini" amemalizia. 
 Mchungaji  Chussi akiongoza sala kabla ya kuanza mkutano wa Watanzania waishio eneo la Bay area- Northen California nchini Marekani waliokutanika jana kukusanya michango ya waathirika wa tetemeko la ardhi lilitokea kanda ya ziwa nchini Tanzania

 Wajumbe wakiendelea na kikao
 Sehemu ya watoto wa  Watanzania waishio eneo la Bay area- Northen California
Mwenyekiti wa jumuiya ya  Watanzania waishio eneo la Bay area- Northen California  Dr Mathias Kaaya akiongoza kikao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mimi nipo in the Bay Area na ni Mtanzania pia. I wish I could get in touch with the rest of the Tanzanians and see how I can donate as well.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...