aziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwigaje akiongea na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Maendeleo  (NDC) wakati akiizindua leo Jijini Dar es Salaam, ambapo ameitaka bodi hiyo kushika miradi mikubwa ya uwekezaji na kuhakikisha inairudisha katika hali yake ili kuiwezesha nchi kufikia uchumi wa kati kupitia uanzishwaji na uendelezaji wa viwanda.
 Wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wakimsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwigaje, wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo, Leo Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwigaje(kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Taifa Maendeleo (NDC) Dkt. Samweli Nyantahe nyaraka mbalimbali zitakazomuongoza katika utendaji kazi.
 Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwigaje akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Taifa la Maendeleo  (NDC) mara baada ya kuizindua leo Jijini Dar Es Salaam.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
WAZIRI wa Viwanda ,Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema Shirika la  Taifa Maendeleo ya Viwanda (NDC) ndio injini ya kushikiria sekta ya viwanda na hivyo inatakiwa kuhakikisha ndani ya miaka minne inakuwa  viwanda hata vitatu katika kuweza kufikia uchumi wa kati.

Mwijage ameyasema hayo leo wakati wa Uzinduzi wa BAodi mpya ya Wakurugenzi NDC, amesema kuwa bodi lazima ifanye kazi kuhakikisha inashikiria viwanda vikubwa ambayo vitafanya taifa kuwa na maendeleo ya kiuchumi kutokana miradi iliyopo chini ya NDC.

Amesema kuwa mradi wa kwanza ni ule wa Liganga na Mchuchuma unatakiwa kufutika midomoni  mwa watu kwa kuanza kuzalisha kutokana na muda mrefu umekuwa ukizungumzwa.

Mwijage amesema kuwa  kutokana bodi hiyo kuwa na watu wa kila sekta muhimu hivyo wanahitaji kukutana mara kwa mara hata bila kulipwa posho ili mambo yeande na kuleta tija kwa taifa.

Amesema kuwa miradi mikubwa ikikamilika nchi itakuwa imepiga hatua kimaendeleo na kuweza kufikia uchumi wa kati  wa viwanda vyenye kwa wananchi.

Nae Mwenyekiti wa bodi wa NDC,  Dk, Samwel Nyantahe amesema kuwa watafanya kazi kwa karibu na wizara ikiwa ni pamoja na kutembelea miradi yote na kuweza kuanza kufanya kazi kwa nguvu.
Amesema Rais Dk. John Magufuli amemuamini hivyo watatimiza wajibu kwa kushirikiana na bodi hiyo katika sekta ya viwanda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...