Na Raymond Mushumbusi WHUSM.

Mashabiki wa soka nchini wameondolewa wasiwasi kuhusu upatikanaji wa tiketi kuelekea mchezo wa ligi Kuu Tanzania Bara kati ya watani wa Jadi Yanga na Simba na kuhakikishiwa kuwa mfumo wa upatikanaji tiketi uko vizuri na mpaka sasa tiketi zinaendelea kuuzwa katika maeneo mbalimbali.

Wasiwasi huo umetolewa na Waziri wa Habari Utamaduni sanaa na Michezo  Mhe. Nape Moses Nnauye alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu matumizi ya tiketi za kieletroniki kuelekea mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara kati ya Yanga na Simba.

Waziri Nape amesema kuwa kuna kuna taarifa kutoka mitaani kuwa kuna uwezekano wa mfumo huu kutofanya kazi katika mechi hii na malalamiko ya watu wengi kulalamika kukosa tiketi za mchezo wa kesho.

“kwa kila anayetaka kwenda uwanjani kesho kadi zinapatikana nimewaagiza Selcom wahakikishe wanazungusha magari yao mtaani kuangalia mahali penye upungufu na yawe na watu wenye kadi hizo aidha, watu waongezwe kwenye vituo ambayo vina idadi kubwa ya wateja wanaohitaji kadi” Alisema Mhe Nnauye.

Aidha Waziri Nape Nnauye amewahakikishia watanzania kuwa atausimamia mfumo huu kikamilifu na kwa gharama yoyote na atahakikisha   hautakuwa na mapungufu na endapo yatajotokeza yatashughulikiwa na wataalamu ili kuufanya mfumo huu kufanya kazi ipasavyo kama ulivyokusudiwa.

Kwa upande wake Meneja Mradi kutoka Selcom Tanzania Galius Runyeta amefafanua kuwa mfumo huu uko wazi kabisa kwa wadau wote wanaohusika na mapato ya uwanjani na utakuwa njia mbadala ya kudhibiti mapato yatokanayo na mechi.

“ Kwa mfumo huu hakuna njia ya mkato kila kitu kiko wazi na kwa kila dakika utaona mabadiliko ya idadi ya tiketi zinazonunuliwa na mpaka sasa zaidi ya tiketi 10,000 zimenunuliwa na zinazidi kununuliwa” Alisema Runyeta.

Kwa miaka mingi kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wadau wa soka nchini kuwepo kwa upotevu wa mapato katika mechi za ligi na kimataifa katika viwanja vya soka nchini kwa kuliona hilo Serikali iliamua kuanzisha mfumo utakaomaliza tatizo hilo na kukomesha mianya yote ya ulaji iliyokuwepo katika mfumo uliopita. 
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam kuhusu maendeleo ya upatikanaji  wa tiketi za kieletroniki  kuelekea mechi ya Ligi kuu Tanzania Bara ya watani wa Jadi  Yanga na Simba itakayochezwa kesho Oktoba Mosi leo ,2016 kushoto ni Meneja Mradi kutoka kampuni ya Selcom Tanzania Bw. Gallius Runyeta.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani)  leo Jijini Dar es Salaam kuhusu maendeleo ya matumizi ya tiketi za kieletroniki  kuelekea mechi ya Ligi kuu Tanzania Bara ya watani wa Jadi Yanga na Simba itakayochezwa kesho Oktoba Mosi leo ,2016. 
 Waziri wa Habari Utamaduni sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akieleza waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es Salaam kuhusu maendeleo ya matumizi ya tiketi za kieletroniki  kuelekea mechi ya Ligi kuu Tanzania Bara ya watani wa Jadi Yanga na Simba itakayochezwa kesho Oktoba Mosi leo ,2016 kulia ni Kaimu kurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara hiyo Bw. Alex Nkenyenge. 
 Meneja Mradi kutoka kampuni ya Selcom Tanzania Bw. Gallius Runyeta akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Jijini Dar es  Salaam jinsi ya kutumia  mfumo kununua tiketi za kieletroniki  kuelekea mechi ya Ligi kuu Tanzania Bara ya watani wa Jadi Yanga na Simba itakayochezwa kesho Oktoba Mosi leo ,2016. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...