Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa akielekezwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula (Mb). na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mipango Miji na Vijiji, Immaculate Senje kutumia mashine ya ATM kwa ajili ya kupata huduma katika Kituo cha Huduma kwa Mteja – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Waziri huyo amefika nchini kujifunza Utawala wa Ardhi.
Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa akiwa ameambatana na ujumbe wake ndani ya Kituo cha Huduma kwa Mteja – Wizarani, akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mipango Miji na Vijiji, Immaculate Senje, akipewa maelekezo na mtumishi jinsi huduma zinavyotolewa katika Kituo hicho. Waziri huyo amefika nchini kujifunza Utawala wa Ardhi. 
Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa akikabidhi Dola 300 kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Kurui – Kisarawe, kama pongezi kwa kijiji hicho kuwa mfano bora katika Mpango wa Utekelezaji wa Matumizi bora ya Ardhi. Waziri huyo amefika nchini na ujumbe wake kujifunza kuhusu Utawala wa Ardhi.
Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa akimpa mkono wa pongezi Mwenyekiti wa kijiji cha Kurui – Kisarawe, kama pongezi kwa kijiji hicho kuwa mfano bora katika Mpango wa Utekelezaji wa Matumizi bora ya Ardhi. Katika picha ya pamoja na Watendaji mbalimbali wa Sekta ya Ardhi na ujumbe ulioambatana na Waziri kufika nchini kujifunza kuhusu Utawala wa Ardhi.
Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa akiwa amewasili Ofisini kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi, akiwa ameambatana na ujumbe wake, uliofika nchini kujifunza kuhusu Utawala wa Ardhi. 
Waziri wa Maendeleo ya Miji na Vijiji wa Namibia; Sophia Shaningwa, katikati akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ; Angeline Mabula, kushoto kwake. Kulia kwake ni Kaimu Kamishna wa Ardhi ; Mary Makondo na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Mipango Miji na Vijiji, Immaculate Senje pamoja na wajumbe walioambatana na Waziri huyo wa Namibia, waliofika nchini kujifunza kuhusu Utawala wa Ardhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...