Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Alex Nkenyenge(katikati) akionyesha mchoro wa mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Taifa na Uwanja wa Uhuru kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy leo Jijini Dar es Salaam,kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa WADIDEGLA upande wa Afrika Bw.Rami Nashed.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi. Joyce Hagu (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo ya mchoro wa mradi wa kituo cha utamaduni kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Petro Lyatuu (kulia)akieleza jambo kwa Rais na Mwanzilishi wa WADIDEGLA kutoka Misri Bw. Adel Samy (kushoto), baada ya kikao kilichojadili masuala mbalimbali ya namna ya kuwezesha ushirikiano wa kuendeleza sekta zilizo chini ya wizara leo Jijini Dar es Salaam. 


Wajumbe wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo pamoja na wajumbe kutoka WADIGLA Misri wakifuatilia kwa makini fursa video iliyokuwa ikionyesha fursa mbalimbali zinazotolewa na WADIDEGLA Misri ikiwemo fursa katika sekta ya Michezo yenye lengo la kukuza na kuendeleza michezo mbalimbali. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...