Katika kusherehekea sikukuu ya Idd el Hajj, Kampuni ya simu ya ZANTEL kupitia Promosheni yake ya Jibwage na mbuzi, imewazawadia wateja walioshiriki promosheni hiyo jumla ya mbuzi 400, kwa ajili ya kuchinja ikiwa ni sehemu ya kusherehekea sikukuu ya Idd ya kuchinja.

Washindi hao walipatikana kufuatia wateja 400 wa kwanza kutumia dakika nyingi zaidi katika simu zao. Mbali na kuwakabidhi washindi hao, Kamuni hiyo haikuwasahau Watoto Yatima, ambapo ilitoa Mbuzi100 katika vituo mbali mbali vya watoto Yatima nchini.

Vituo hivyi ni pamoja na Children's Home, Tanzania Mitindo House, na vituo vingine vilivyo chini ya uangalizi wa BAKWATA, vituo vingine ni vya Tanga, Mtwara na Lindi , Unguja na Pemba.
Mkuu wa Kampuni ya Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa Baucha (wa pili kulia) akikabidhi mbuzi kwa washindi wa promosheni ya jibwage na mbuzi visiwani Zanzibar jana.
Afisa Habari na Mawasiliano wa Zantel, Winnes Lyaro (wa pili kushoto) akikabidhi mbuzi mshindi Bi. Zulfa mkazi wa Dar huku wateja wengine waliopata nafasi ya kujizawadia mbuzi wakiwa katika picha ya pamoja. Zantel imewezawadia wateja wake 400 nchini waliotumia dakika nyingi zaidi katika ofa ya wiki mbili ya Jibwage na Mbuzi iliyoandaliwa rasmi na kampuni hiyo ili kuwazawadia wateja wake mbuzi kipindi cha sikukuu huku mbuzi 100 kati ya hao wakiwazawadia watoto yatima nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...