Mtangazaji maarufu aliyewahi kutangaza kituo cha redio cha Clouds Fm nakujiunga na EFM redio na baadaye kurudi tena Clouds Fm amefunguliwa mashtaka katika mahakama ya kazi jijini Dar es salaam na EFM redio kwa kile kinachodaiwa kuwa amekiuka mkataba wa kazi wa kituo hicho.

Kufuatia mashtaka hayo, Efm inadai fidia ya shilingi milioni 200 kwa mtangazaji huyo ambaye alijiunga na kituo hicho kutoka clouds fm na baadae kudaiwa kukatisha mkataba kiholela na kurudi tena clouds fm bila kufuata makubaliano pamoja na sheria alizokubaliana nazo katika mkataba wake awali wakati  alipojiunga na efm redio.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tarehe 23/11/2016 katika mahakama ya kazi Jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...