Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika, Issa Hayatou ameteua Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa miongoni mwa wajumbe 11 wa Kamati maalumu ya mageuzi ya muundo wa CAF itakayokuwa na jukumu la kufanya mabadiliko mapya ya shirikisho, imefahamika.

 Kwa mujibu wa taarifa ya CAF, katika Kamati hiyo ikayoongozwa na Rais Issa Hayatou mwenyewe, Malinzi ameteuliwa katika Kamati hiyo iliyotangazwa leo Oktoba 30, 2016 kutoka ukanda wa Afrika Mashariki.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://tff.or.tz/news/648-hayatou-amteua-malinzi-kamati-ya-mageuzi-caf

Wakati huo huo

LIGI YA TAIFA WANAWAKE KUANZA RASMI KESHO

Ligi ya Taifa ya Wanawake inatarajiwa kuanza kesho Jumanne Novemba 1, 2016 kwa viwanja sita kuchezwa mechi za ufunguzi ingawa hafla ya uzinduzi wa ligi hiyo utafanyika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma katika mchezo ambao Baobao ya hapo itakapocheza na Victoria Queens ya Kagera.

Ligi hiyo ya kwanza kufanyika nchini Tanzania, lakini pia kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati imetokea kuvutia wadau kadhaa wakiwamo Azam Tv ambao wamedhamini kwa kuonyesha mubashara (live), michezo hiyo 30 itakayofanyika viwanja mbalimbali hapa nchini.

Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...