Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika, Issa Hayatou ameteua Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kuwa miongoni
mwa wajumbe 11 wa Kamati maalumu ya mageuzi ya muundo wa CAF
itakayokuwa na jukumu la kufanya mabadiliko mapya ya shirikisho,
imefahamika.
Kwa
mujibu wa taarifa ya CAF, katika Kamati hiyo ikayoongozwa na Rais Issa
Hayatou mwenyewe, Malinzi ameteuliwa katika Kamati hiyo iliyotangazwa
leo Oktoba 30, 2016 kutoka ukanda wa Afrika Mashariki.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
http://tff.or.tz/news/648- hayatou-amteua-malinzi-kamati- ya-mageuzi-caf
Wakati huo huo
Wakati huo huo
LIGI YA TAIFA WANAWAKE KUANZA RASMI KESHO
Ligi ya Taifa ya Wanawake inatarajiwa kuanza kesho Jumanne Novemba 1, 2016 kwa viwanja sita kuchezwa mechi za ufunguzi ingawa hafla ya uzinduzi wa ligi hiyo utafanyika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma katika mchezo ambao Baobao ya hapo itakapocheza na Victoria Queens ya Kagera.
Ligi hiyo ya kwanza kufanyika nchini Tanzania, lakini pia kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati imetokea kuvutia wadau kadhaa wakiwamo Azam Tv ambao wamedhamini kwa kuonyesha mubashara (live), michezo hiyo 30 itakayofanyika viwanja mbalimbali hapa nchini.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...