Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida (kulia) na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Flora Rajabu Yongolo, wakisaini hati za makubaliano ya msaada wa shilingi za Tanzania milioni 170 uliotolewa na Serikali ya Japan kusaidia Mradi wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Murangi kilichopo wilayani Musoma, mkoani Mara. Wanaoshuhudia (waliosimama) ni Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Flora Rajab Yongolo, akitoa neno la shukrani kwa Serikali ya Japan kwa msaada uliotolewa.
Waziri wa Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo (aliyeshika kipaza sauti), akimshukuru na kumuaga Balozi wa Japani nchini Tanzania, mara baada ya kuhitimisha hafla ya kutia saini makubaliano ya msaada utakaosaidia upanuzi wa kituo cha afya cha Murangi kilichopo wilayani Musoma, Mkoa wa Mara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...