’Wito watolewa kwa kila mwananchi kuwajibika kwa malengo ya Dunia’
OKTOBA 24 kila mwaka Umoja wa Mataifa hufanya maadhimisho ya kuzaliwa kwake.
Mwaka
huu mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania kwa kushirikiana na
serikali, wadau wa maendeleo na vijana wataadhimisha miaka 71 ya uwapo
wa Umoja wa Mataifa kwa staili ya aina yake.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa katika mkutano wa waandishi wa habari na
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ikishirikiana
na Umoja wa Mataifa , maadhimisho hayo mwaka huu yamelenga kuelezea kwa
undani shughuli zinazofanywa kwa pamoja kati ya pande hizo mbili ili
kuwezesha maendeleo endelevu.
Katika
mkutano huo wa pamoja, waandishi wa habari walielezwa kwa ufupi Mpango
Mpya wa Maendeleo Chini ya Ufadhili wa Umoja wa Mataifa ( UNDAP ll -2016
hadi 2021) kwa serikali ya Tanzania; na mpango wa maendeleo wa miaka
mitano wa Tanzania ambamo malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kama
yalivyosanifiwa na kukubalika na jumuiya ya kimataifa, yameshirikishwa.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt.
Augustine Mahiga akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani)
katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es
Salaam. Mhe. Balozi Dkt. Mahiga, amezungumzia umuhimu wa maadhimisho wa
Siku ya Umoja wa Mataifa na faida za Jukwaa la umoja huo kwa maendeleo
ya Taifa. Maadhimisho hayo yatafikia kilele tarehe 24 Oktoba,
2016.(Picha zote na Reginald Kisaka wa Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki).
Katika
mkutano huo na waandishi wa habari pia kulikuwepo na majadiliano ya
mafanikio ya shughuli za Umoja wa Mataifa hadi sasa duniani na pia
nchini Tanzania .Pia mazungumzo hayo yalijikita katika malengo ya
Maendeleo Endelevu (SDGs) na umuhimu wa malengo hayo kumilikishwa kwa
wananchi na wajibu wao katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na utekelezaji
wenye mafanikio.
Pia
ilielezwa katika mkutano huo kwamba maadhimisho ya miaka 71 ya Umoja wa
Mataifa, Siku ya Umoja wa Mataifa, yatafanyika katika viwanja vya
Karimjee jijini Dar es Salaam Oktoba 24.Maadhimisho hayo ambayo mwaka
huu yamebeba ujumbe wa :“Uwezeshaji wa vijana Tanzania kufikia malengo
ya dunia” yanafanyika huku kukiwa na malengo mapya ya dunia ya maendeleo
endelevu.Malengo hayo ya SDGs yamelenga kuondoa umaskini kwa kuwa na
maendeleo endelevu.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt.
Augustine Mahiga katika mkutano na waandishi wa habari.
Aidha
ujumbe huo unaenda sanjari na mpango wa maendeleo wa awamu ya pili wa
Umoja wa Mataifa kwa Tanzania (UNDAP II) ambao unaendeleza ule wa awali
wa kuanzia 2011-16 ukiwa umejikita katika masuala ambayo ni muhimu
kwenye kukabili umaskini kwa kuwa na maendeleo endelevu.
Maadhimisho
ya mwaka huu yalitanguliwa na kongamano la vijana wapatao 200, ambao
walijadili masuala yanayogusa fursa za uchumi na maendeleo ya jamii na
mchango ambao unaoweza kutolewa na vijana kufanikisha utekelezaji wa
malengo hayo.
Maadhimisho
hayo yatafikia kilele chake nchini kwa tukio litakalofanyika Visiwani
Unguja Oktoba 26 mwaka huu.Imeelezwa kuwa maadhimisho ya mwaka huu
yanaonesha uwapo wa ushirikiano mkubwa na wenye tija kati ya Tanzania,
wananchi wake na Umoja wa Mataifa.
Kaimu
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bi.Chansa Kapaya
akizungumza na waandishi wa habari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...