Na  Bashir  Yakub.
Mtu  anapokufa  huacha  warithi  wa  namna  mbalimbali.  Yumkini  ndani  mwake  waweza  kuwamo  watoto  wenye  umri  mdogo na  hata  vichaa.  Umri  mdogo  twaweza  kuuhesabu  kuanzia   mwaka  0  mpaka 18. Aidha wakubwa ambao  wamezidi  miaka 18  hao nafasi  yao   inajulikana   ikiwa  marehemu  ameacha  mali.

Mali  zao  watakabidhiwa  kwa  utaratibu  maalum  ulioratibiwa  na  sheria.  Swali  litakuwa  kwa watoto wadogo  ambao  hawawezi  kukabidhiwa, tutahitaji  kujua  sheria  inasemaje.
Hapa  kuna  mazingira  ya aina  mbili kwanza, ni  pale marehemu  anapoacha  warithi  watoto  tu  na  hakuna  mkubwa  hata  mmoja  na  pili ni  pale anapoacha  warithi wakubwa  na  watoto.

Pia  kwa  ufupi  tutaangalia   sheria  inavyosema  kuhusu  mali  za  mrithi  ambaye  hana  akili  timamu. Hii  nayo  tutaangalia  mazingira  yote,  mazingira  anapokuwa  na  warithi  wenzake  na  mazingira  anapokuwa  mrithi  pekee.

1.MTOTO  MDOGO.
Sura  ya  352 kifungu  cha  23 Sheria  ya  mirathi  kinasema  kuwa  urithi  au  hati  ya  kusimamia  mirathi  haiwezi  kutolewa  kwa  mtoto mdogo.

Tukiachana  na hilo tujue  kuwa  ikiwa mtoto  mdogo  si  mrithi  pekee  isipokuwa  wapo  ndugu  zake  wengine  ambao  ni  warithi  basi  mmoja  wao  muadilifu  atateuliwa  kusimamia  mirathi  yote ikiwemo  ya  mtoto  mdogo. Msimamizi  huyo  atakuwa  na  wajibu  wa  kuhakikisha  anatunza  mali  ya  mtoto/watoto  hao  mpaka  wanakua  na  kuwa  na uwezo  wa  kutunza  mali  zao  binafsi.

Pili ni  pale  ambapo  mtoto/watoto  wadogo  ndio  warithi  pekee   wa  mali yaani  hakuna  mkubwa  kati  yao.  Ikiwa  hilo  litatokea  basi   mlezi  wa  watoto anaweza  kuomba  mahakamani  kusimamia  mirathi hadi  watakapokua.

Taasisi  ya  udhamini  ( trust  cooperation)  pia  yaweza  kuomba  au  kupewa  bila  kuomba  jukumu  la kusimamia  mali  za watoto  hadi  watakapokua. Hii  ni  kutoka  kifungu  cha 22 cha  sheria  ya  mirathi.  Yeyote  atakayeteuliwa  kati  yao  atakuwa na  wajibu  mkubwa wa  kuhakikisha  anatunza  mali  za  watoto  kwa  kadri  mahakama itakavyoelekeza.

Wakati  mwingine  wanaweza  kujitokeza  walezi   wengi  kila mmoja  akitaka  kusimamia  mali  za  watoto.  Ikiwa  itakuwa  hivyo  basi  suala  hilo  litapelekwa  mahakamani  na  mahakama  itaamua  nani  anafaa  kusimamia  mali  hizo  kwa  kuzingatia  zaidi  mustakabali  wa  baadae  ya  hao  watoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...