Mtangazaji wa Kipindi cha "The Mboni Show" kinachoruka
kupitia kituo cha televisheni TBC1, Mboni Masimba ameandaa kongamano la
kuwahamasisha wanawake aliloliita Sauti
ya Mwanamke lenye lengo la kuwapa uwezo wa kujikomboa kiuchumi.
Katika kongamano hilo
litakalofanyika mkoani Mwanza Novemba 6, mwaka huu katika Hoteli ya Gold Crest,
wanawake mbalimbali waliofanikiwa
kiujasiriamali, kibiashara na kielimu watakuwepo kuzungumza na wanawake wa jiji hilo kwa kiingilio cha Sh40,000.
Masimba anasema kwa kiingilio hicho wanawake wa Mwanza
watapata elimu, burudani pamoja
na chakula.
"Atakuwepo Shekha Nasser ambaye ni mmiliki wa Shear Illusion na
Mwanzilishi wa Manjano Foundation huyu amefanikiwa sana kwenye biashara, atakuwepo
Mkandarasi Maida Waziri pamoja na Biubwa Ibrahim ambaye ana Kampuni ya Namaingo Agri_Busness Agency inayowawezesha
watu mbalimbali katika masuala ya kilimo," amefafanua Masimba.
Anaongeza kuwa pamoja na kupata elimu ya biashara na ujasiriamali,
maarifa kuhusu maisha na nyumba yatatolewa na wawezeshaji maarufu Bi Chau na Bi
Fatma.“Wanawake mnapokutana lazima mbadilishane ujuzi wa kila aina,
hatutawaacha hivi hivi wanawake wa Mwanza, tumemuandaa Bi Chau na Bi Fatma
kuwafunda yale mambo yetu,” anafafanua.
Shughuli yoyote ya wanawake bila burudani haiwezi kunoga ndiyo maana
Masimba anawapeleka Mwanza, Isha Mashauzi na mchekeshaji Katarina Karatu
kuifanya siku hiyo iwe nzuri.Masimba anasema sherehe itaendeshwa na mshereheshaji maarufu nchini Mc
Zipompapompa.
“Tunaanzia Mwanza, lakini kongamano letu litakwenda nchini kote,
tunataka kuwakomboa kifikra wanawake wa Kitanzania, Sauti ya Mwanamke ni sauti ya jamii, ipewe nafasi,” anasema
Masimba.
ticket zinatikana wapi?muda?
ReplyDelete