NA VICTOR  MASANGU, RUFIJI.

BAADHI ya wakinamama wajawazito wanaoishi katika vijiji vya  Mbunju na Mbambe vilivyopo kata ya Mkongo. Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya muda mrefu ya kujifungulia wakiwa  njiani kutokana na kuwepo kwa umbali mrefu kutoka makazi wanayoishi hadi kufika katika zahanati au  kituo cha afya kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Wakinamama hao wametoa kilio chao wakati walipotembelewa na mbunge wa jimbo la Rufiji ikiwa ni moja ya ziara yake ya kikazi yenye  lengo la kuweza kusikiliza changamoto  mbali mbali zinazowakabili wananchi wake  pamoja na  kero zao  ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi na kuweka mikakati ya kuleta chachu ya maendeleo.

Zarau Kiambwe  Tabia Athumani,pamoja na Suzan Masela  ni miongoni mwa wakinamama hao wanaokabiliwa na changamoto hiyo,walisema  wakati mwingine wanapata wakati mgumu hususan nyakati za usiku kutokana na kukosa usafiri hivyo kuwalazimu kujifungulia njiani hali ambayo inahatarisha uhai wa kupopteza maisha yao ukizingatia na gharama za usafiri wa piki piki ni kubwa hivyo wanashindwa kuzimudu kutoka na kutokuwa na kipato chochote.

Aidha wakinamama hao wamemuomba Mbunge wa jimbo hilo la Rufiji kwa kushirikianana serikali ya awamu ya tano kuliingilia kati suala hilo ili kuweza kuwasaidia wananchi kwa  kuwajengeaa  zahanati pamoja na vituo vya afya vilivyvyo karibu na maeneo wanayoishi ili kuweza kupata huduma ya matibatu kwa urahisi bila ya  usumbufu.

 Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa akizungumza na wananchi wa vijiji vya Mbunju na Mbambe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuwatembelea kwa ajili ya kuweza kubaini changamoto mbali mbali zinazowakabili ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.(PICHA NA VICTOR MASANGU).
 Mbunge wa jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa akizungumza na baadhi ya wanakijiji hicho kwa ajili ya kuweza kujadili kero zinazowakabili.
 Mbunge wa Rufiji akifurahia jambo baada ya mzee maarufu kijijini hapo kumpa pongezi za dhati kwa kuhudi zake anazozifanya katika kuwataumikia wananchi wa jimbo hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...