Na Mathias Canal, Singida
Zao la Pamba ni miongoni mwa mazao ya kipaombele ya biashara
yanayozaliswa Mkoani Singida kwa kuwa linastahimili hali ya hewa ya Mkoa ya
uwepo wa mvua zenye mtawanyiko usioridhisha kwa baadhi ya maeneo ambapo
kutokana na hali hiyo Mkoa unaendelea kuhimiza wakulima kuzalisha zao hilo kwa
kiasi kikubwa ili waweze kuongeza kipato na usalama wa chakula.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Mkutano wa wadau wa kilimo
cha pamba Mkoa wa Singida ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew
Mtigumwe wakati akifungua Mkutano huo iliokuwa na dhamira ya kujadili maendeleo
ya kilimo cha zao la Pamba katika mkoa huo.
Mhe Mtigumwe amesema kuwa Katika Mkoa wa Singida Kampuni ya
Biosustain Ltd inayojishughulisha na Kilimo cha Mkataba imeweza kusaidia zao la
Pamba kwa kuanzisha kiwanda cha kuchambua Pamba chenye uwezo wa kuchambua Tani
16,000 kwa mwaka ambapo kupitia kilimo cha mkataba wakulima wa Mkoa wa Singida
wamepata pembejeo, Mafunzo ya kilimo bora na soko la uhakika ambapo katika
utekelezaji wa kilimo cha mkataba msimu wa mwaka 2015/2016 wakulima 4,204
wamepatiwa mafunzo.
Kwa msimu huu wa Mwaka 2016/2017 Mkoa umepata mgao wa mbegu
za Pamba kutoka Bodi ya Pamba jumla ya Tani 120 (Wilaya ya Iramba na Mkalama
Tani 80, Wilaya ya Manyoni Tani20 na Wilaya Ikungi na Singida Tano 20) ambazo
zinaendelea kusambazwa kwa wakulima.
Imeelezwa kuwa zao la Pamba linakabiliwa na changamoto
mbalimbali ikiwemo tija ndogo katika uzalishaji (200 kg/ekari) kutokana na
wakulima kutozingatia kanuni bora za kilimo cha pamba, matumizi ya viuatilifu
ambavyo havina uwezo wa kudhibiti wadudu waharibifu wa zao la pamba (Feki),
Matumizi ya mbegu zisizoota vizuri (Feki), Kubadilika kwa bei ya pamba mwaka
hadi mwaka, Mvua zenye mtawanyiko usioridhisha kwa baadhi ya maeneo kwa mfano
maeneo ya Bonde la Ufa ya Iramba, Mkalama na Manyoni.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew Mtigumwe akifungua Mkutano wa wadau wa pamba wenye dhamira ya kujadili maendeleo ya kilimo cha zao la Pamba katika mkoa wa Singida.
Wadaau wa kilimo cha Pamba Mkoa wa Singida wakifuatilia kwa makini Mkutano wa kujadili namna bora ya kuimarisha kilimo cha zao hilo katika Mkoa wa Singida
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa wadau wa pamba Mkoa wa Singida
Wadaau wa kilimo cha Pamba Mkoa wa Singida wakifuatilia kwa makini Mkutano wa kujadili namna bora ya kuimarisha kilimo cha zao hilo katika Mkoa wa Singida.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...