Rais wa Korea Kusini, Park Geun-hye amemtunuku nishani ya heshima aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Bw.Henry Clemens kwa kutambua juhudi zake katika kuleta maendeleo katika vijiji vya Mfuru Mwambao na Njianne kupitia mfumo Saemaul Undong (SMU) yaani kijiji kipya cha maendeleo.

SMU ni mfumo uliotumika Korea katika kujiletea maendeleo mpaka sasa kufika katika orodha ya nchi tajiri duniani. Mfumo huo unasisitiza swala la wananchi wenyewe kufanya kazi kwa kujitolea kwa ajili ya maendenelo yao wenyewe.Bw. Clemens ambaye ni mwenyekiti wa SMU Tanzania alisema wazo hilo alilipokea mwaka 2009 akiwa Mkuu wa wilaya ya Mkuranga na kulifanyia kazi katika vijiji viwili na kuleta matokeo mazuri.

“kumekuwa na maendeleo makubwa mara baada ya kutoa mafunzo kwa wanakijiji juu ya thamani ya ardhi na umuhimu wa kufanya kazi kwa ushirikiano,” alisema Bw. Clemens.Alisema uzalishaji wa mazao kama mhogo, papai na nazi umeongezeka kwa asilimia kubwa kutokana na ushirikiano wa wanavijiji wa Mfuru Mwambao na Njia nne.
Mwenyekiti wa Saemaul Undong Tanzania(SMU), Bw.Henry Clemens akikambidhi zawadi kwa niaba ya wanakijiji wa Njianne, wilayani Mkuranga Balozi wa Korea Kusini Nchini Bw.Song Geum-young alipotembelea katika kijiji hicho kujionea maendeleo waliofikia kwa kupitia dhana ya Saemaul Undong yaani kijiji kipya cha maendeleo ambayo ndio dhana iliyowafanya wao kupiga hatua kiuchumi mpaka kufikia katika prodha ya nchi tajiri Duniani. Katikati ni mwasisi wa SMU Mchungaji Joshua Lee
Mwenyekiti wa Saemaul Undong Tanzania,(Mkuu wa Wilaya Mstaafu wa Mkuranga) Bw.Henry Clemens akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) medani ya heshima na cheti alichokabidhiwa na Rais wa Korea kusini Park Geun-hye kwa kutambua mchango wake wa kuviendeleza vijiji vya Mfuru mwambao na Njia nne vilivyopo Wilaya ya Mkuranga kupitia mfumo wa saemaul undong( kijiji kipya cha maendeleo).
Balozi wa Korea Kusini Nchini Tanzania Bw.Song Geum-young akipiga picha daraja linalounganisha kijiji cha Njia nne na Nyamihimbo wakati waziara yake katika kijiji hicho na kujionea maendeleo waliofikia kwa kupitia dhana ya Saemaul Undong yaani kijiji kipya cha maendeleo ambayo ndio dhana iliyowafanya wao kupiga hatua kiuchumi mpaka kufikia katika prodha ya nchi tajiri Duniani. Kulia ni Mbunge mstaafu wa Mbinga Magharibi Bw.Gaudence Kayombo. Kushoto ni mwasisi wa SMU Tanzania,Mchungaji Joshua Lee. Wapili kushoto Mwenyekiti wa Saemaul Undong Tanzania Bw.Henry Clemens

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...