Na Eleuteri Mangi, WHUSM

Mataifa wanachama wa Umoja wa Mataifa (UN) yanashiriki kwenye shughuli mbalimbali za kijamii kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 71 ya umoja huo kinachofikia Oktoba 24 mwaka huu baada ya kuasisiwa kwake mwaka 1945.

Tanzania ambayo ni mwanachama hai wa UN imeungana na umoja huo kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali za kuunganisha nguvu za vijana na kuwajenga kimaadili, kiuchumi ili waweze kujitambua na kujua mustakabali wao katika kujenga uchumi wa nchi.

Kwa kuwa vijana ni nguzo kuu ya kujenga taifa lolote duniani, Tanzania kwa kukushirikiana Umoja wa Mataifa imeona umuhimu wa kuwashirikisha vijana kupitia kongamano la vijana kutoka shule za sekondari na vyuo vikuu nchini lililofanyika Oktoba 18 mwaka huu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) uliopo jijini Dar es salaam.

Lengo la kongamano hilo ni kuwashirikisha vijana kujadili namna watakavyoshiriki katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na kutafuta namna bora ya kutatua changamoto zinazowakabili vijana nchini.

Vijana hao wamepata fursa ya kukumbushana, kuelimishana na kubadilishana mawazo juu ya namna bora inayowawezesha kutoa mchango wao katika masuala ya kiuchumi na maendeleo ya kijamii nchini.

Kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Viana ya mwaka 2007, ujana ni kundi mtambuka ambalo linajumuisha vijana kuanzia miaka 15 hadi 35 ndio maana wanaitwa ni nguvu kazi ya taifa kwa kuwa wengi wao kuanzia miaka 18, umri wa mtu mwenye nguvu na uwezo mzuri wa kufikiri na kuchangia katika maendeleo ya taifa kiuchumi na kijamii.

Akifungua kongamano hilo, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel amewaasa vijana kuwa watakumbukwa kwa mchango wao watakaotoa kwa jamii na si kwa nafasi zao kwa kuchangia uchumi na maendeleo ya nchi, hivyo ni wajibu watambue umuhimu wao kwa taifa.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifungua kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam wakati wa wiki ya maadhimisho ya Umoja wa Mataifa unaofikisha miaka 71 tangu kuasisiwa kwake. Maadhimisho ya hayo yanaongozwa na kaulimbiu kwa upande wa Tanzania inayosema “Jukumu la Vijana wa Tanzania katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii”.

Mwakilishi wa Shirika Umoja wa Mataifa nchini linaloshughulikia Maendeleo (UNDP) Annamaria Kiaga akimkaribisha Mgeni Rasmi ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel kufungua kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam

Baadhi ya washiriki wa kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam wakati wa ufunguzi wa kongamano la vijana lililoandaliwa na Shirika Umoja wa Mataifa linalishughulikia Maendeleo (UNDP).

Baadhi ya washiriki wa kongamano la vijana kutoka shule na vyuo mbalimbali nchini wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel Oktoba 18, 2016 jijini Dar es salaam wakati wa ufunguzi wa kongamano la vijana lililoandaliwa na Shirika Umoja wa Mataifa linalishughulikia Maendeleo (UNDP).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...