Editha Karlo,wa blog ya jamii,Kagera.

RAIS John Pombe Magufuli amesema kuwa serekali ipo pamoja na wanakagera katika kipindi hiki ambacho  wamekumbwa na tetemeko la ardhi na lililopelekea kuleta maafa na kupoteza makazi.

 Magufuli aliyasema hayo jana kwenye viwanja vya seminari ya Rubya wakati wa ibada ya misa ya uzinduzi wa jubilei ya miaka 150 uinjilishaji na 100 ya upadre Tanzania.

Waziri wa viwanda biashara na uwekezaji,Mh Charles Mwijage  aliyasema hayo kwa niaba ya Rais, alisema kuwa Rais amemtuma kuwapa pole nyingi wana kagera walioathirika na tetemeko la ardhi lililotokea september 10 mwaka huu.

 Magufuli alisema kuwa serekali yake inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuboresha miundombinu mbalimbali kwa haraka kama vile shule,zahanati,nyumba za ibada na barabara ili huduma za kijamii ziwe kurudi katika hali yake ya kawaida.

 Aliwapongeza wanakagera kwa uvumilivu waliounyesha katika kipindi hiki walichokumbwa na tetemeko la ardhi ambapo hawajayumba kiimani wameendelea kusimama imara.8

 " Sasa hivi mataifa mbalimbali na Dunia kwa ujumla pamoja na Serekali yangu ipo bega kwa bega na wanakagera katika kuhakikisha miundo mbinu iliyo haribiwa na tetemeko ina rudi haraka katika hali yake ya awali"alisema Magufuli.

 Pia Rais Magufuli alilipongeza kanisa katoliki kwa mchango wake mkubwa katika huduma za kijamii kama vile elimu,afya pamoja na huduma zingine  xa kijamii wamekuwa wakifanya vizuri na serekali inautambua mchango wao.

 Naye Askofu mkuu wa jimbo la Mwanza Thadeus Rweiche kwaniaba ya Rais wa baraza la maaskofu Tanzania(TEC) Talicusis Ngaralekumtwa aliwataka wanakagera kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha mpito na kuwataka mapdre wasivunje moyo katika kazi zao za unjilishaji.

Alisema huduma za kiroho zinatolewa katika mazingira mazuri kwasababu serekali inatoa ushirikiano wa bega kwa bega na viongozi wa dini pamoja na waumini.

 Askofu Rweiche alisema semenari ya Rubya ni chimbuko la mapdre kwa Afrika mashariki.
 Waziri wa viwanda na biashara Charles Mwijage akitoa salamu za Rais John Magufuli kwenye ibada ya misa ya uzinduzi wa Jubilei ya miaka 150 ya uinjilishaji na miaka 100 ya upadre Tanzania iliyofanyika kwenye viwanja vya semenary ya Rubya Wilayani Muleba
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu akitoa salam za Mkoa kwenye ibada ya misa ya uzinduzi wa jubilei ya miaka 150 ya unjilishaji na 100 ya upadre Tanzania
 Katibu mkuu wa baraza la maaskofu Tanzania (TEC)Padre Raymond Saba akitoa neno la shukrani 
 Askofu msaidizi wa jimbo katoliki la  Bukoba Method Kilaini akitoa shukrani kwa niaba ya Askofu mkuu wa Jimbo la katoliki Bukoba Askofu Desderius Rwoma kwa wageni na waumi.wote waliohudhuria ibada hiyo
 Baadhi ya maaskofu kutoka majimbp yote Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya ibada
 Sehemu ya wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania waliohudhuria ibada hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...