KUFUATIA Uhaba wa madawati katika shule za msingi halmashari ya jiji la Tanga na wanafunzi kusomea chini, Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement kimetoa madawati 100 kwa shule tatu. 

Shule hizo ambazo zimefaidika na mpango huo ni Magaoni, Kiruku, Mkombozi na Martini Shamba zote za halmashauri ya jiji la Tanga.
Akizungumza wakati wa makabidhiano mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Tanga , Thobias Mwailapwa, Mkuu wa Idara Rasilimali watu kiwabda cha Saruji , Diana Malambusi amesema msaada huo umekuja baada ya kuona kero ya wanafunzi kusomea chini kutoisha. 


Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano, Mkuu wa Wilaya, Thobias Mwailapwa, amekishukuru kiwanda hicho (Simba Cement) na kuyataka mashirika na taasisi pamoja na makampuni kuiga mfano huo ili kumaliza kero ya wanafunzi kusomea chini. 

Kwa upande wake Afisa elimu shule ya msingi jiji , Khalifa Shemahonge, amesema madawati hayo yatatumika kama inavyokusudiwa na kuahidi kuyatunza ili kuongeza uelewa wa wanafunzi darasani.

Mkuu wa Idara ya Rasilimali watu kiwanda cha Tanga Cement (Simba Cement), Dianna Malambugi (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwailapwa, madawati 100 kwa shule tatu za msingi, Magaoni, Kiruku, Mkombozi na Martin Shamba za halmashauri ya jiji la Tanga kupunguza uhaba wa madawati na wanafunzi kusomea chini.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Thobias Mwailapwa, akimkabidhi Afisa Elimu Shule ya Msingi halmashauri ya jiji la Tanga, Khalifa Shemahonge madawati 100 kwa shule tatu ya, Magaoni, Kiruku, Mkombozi na Martin Shamba yaliyotolewa na kiwanda cha Saruji cha Simba Cementi kupunguza uhaba wa madawati kwa shule hizo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...