SIMU.TV: Uongozi wa jumuiya ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam DARUSO na shirikisho la vyuo vikuu TAHILISO umeonana na waziri wa elimu kutafuta suluhisho la utoaji wa mikopo isiyokidhi haja za wanafunzi. https://youtu.be/_zAn3g3mYb0
SIMU.TV: Waziri mkuu Kassim Majaliwa auagiza uongozi wa mfuko wa hifadhi ya jamii wa NSSF kukusanya madeni yote kwa wadaiwa sugu. https://youtu.be/o2VTu36Cgmw
SIMU.TV: Serikali imeunganisha taasisi 72 katika mtandao wa mawasiliano wa mkongo wa taifa ili kupunguza gharama ya mawasiliano kwa taasisi za serikali. https://youtu.be/SoMGs-yWmxU
SIMU.TV: Serikali imehimiza halmashauri zote nchini kutumia vyanzo vyake vya mapato kununua vifaa tiba kwa ajili ya uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza badala ya kusubiri bajeti ya serikali. https://youtu.be/1awXWiy1avA
SIMU.TV: Wananchi wa vijiji vya Nyabagi na Nyamikoma wameiomba serikali kuwasaidia eneo la makazi ili waweze kuendesha maisha baada ya kuondolewa eneo la hifadhi.https://youtu.be/NG-V4JtNVds
SIMU.TV: Maafisa wa polisi katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam wamemkamata mwanamke mmoja raia wa Brazil kwa kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Cocaine. https://youtu.be/TlNRTkGD16o
SIMU.TV: Wafanyabiashara na watu wenye kipato kikubwa wameshauriwa kuwekeza kwenye masoko ya mitaji na dhamana ili kuibua fursa nyingi kwa wananchi.https://youtu.be/H_ryoApYgRg
SIMU.TV: Waziri wa viwanda na biashara amesema hakuna bidhaa yeyote itakayoingizwa nchini bila kukaguliwa na mamlaka za TBS na TFDA ili kulinda walaji.https://youtu.be/vvjKG7EVTlc
SIMU.TV: Vinara wa ligi kuu Tanzania bara klabu ya Simba imeendelea kufanya vizuri baada ya kuibuka na ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Mbao fc leo. https://youtu.be/Hgu4a-itYdU
SIMU.TV: Mashabiki wa timu ya Majimaji wameipongeza timu yao kwa kuanza kuonesha umahiri kwa kushinda michezo miwili ugenini tangu msimu wa ligi kuu uanze.https://youtu.be/3Vmlw1BSx4o
SIMU.TV: Wachezaji watatu wa timu ya gofu ya Jeshi la ulinzi la wananchi wa Tanzania wameteuliwa kujiunga na timu ya taifa ya gofu. https://youtu.be/S9zau4-aJYU
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...